Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua majukumu makubwa ya Wizara hii katika ujenzi wa Taifa, usalama wa nchi kupitia mipaka ya nchi na usalama wa raia. Malalamiko ya wananchi kwa Jeshi hususani katika maeneo yaliyopakana na Jeshi kwa kigezo cha Jeshi kutokuwa na umiliki halali na wananchi kuingilia maeneo hayo kwa kupewa na Manispaa au Halmashauri na baadae kuleta migogoro ya wananchi kupigwa na wanajeshi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu Wizara ya Ardhi bado inashughulikia mipaka na maeneo hayo yaliyoingiliana na wananchi. Ni kwa nini Jeshi linachukua hatua ya kuwapiga, kuchoma nyumba, kubaka kina mama, kuwapa mateso yasiyoelezeka wananchi ambao kimsingi walipewa maeneo hayo kupitia Halmashauri? Ni kwa nini Jeshi linafanya unyama huu na huku Serikali ikiangalia unyama huu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, mgogoro uliopo katika Kata ya Misunkumilo kuhusu mpaka wa Jeshi jambo hili lipate ufumbuzi. Pia katika Jimbo la Kibamba ambalo Jeshi linaendelea na unyanyasaji kwa raia ni nini suluhisho?