Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna kila sababu ya tuonayo katika hali halisi kwa usimamizi uliotukuka wa Waziri na ushirikiano wa makamanda wake. Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli ambaye ni Jemadari Mkuu mwenye upendo wa Jeshi na nchi yake kwa ujumla na ndiko kunakopelekea amani kuimarika na kudumu nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha za maendeleo zinazopangwa na kuidhinishwa na Bunge ziweze kutolewa katika ukamilifu wake, kwani mwaka 2018/2019 hadi Machi, 2019 zimetolewa asilimia 41.8 ambazo hazitendi haki kwa Jeshi kwani kazi yao ni ngumu na hali hiyo wanahitaji kubadili na kuboresha maeneo yao ipasavyo ili wawe wepesi na katika mazinigira mazuri ya kazi zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la utafiti ni muhimu sana kwani utatuwezesha kufanya mambo yetu kwa ufanisi na tija, kwenye mashirika yetu (Nyumbu na Mzinga) ya Jeshi kuendelea kuwapatia kipaumbele chao. Hivyo tunaomba pesa inayoidhishwa ikatolewa kwa asilimia 85 kuliko hii hali ya asilimia 10 hadi sasa haina mshiko kwa Jeshi letu (2028/ 2019).

Mheshimiwa Mwenyekiti, mgogoro wa wananchi na Jeshi letu la wananchi katika kutwaliwa maeneo na ulipaji wa fidia ni kizungumkuti kwa sasa. Mgogoro huu hauwezi kuwa wa kudumu hapa nchini kwani unatatatulika hivyo unaweza ukatoweka kabisa, kutokutoa pesa inayoidhinishwa kwa ukamilifu na wakati ili waweze kutathimini maeneo hayo na kuyalipia fidia ambayo haiwi na manung’uniko kwa wanaolipwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, malipo ya mwaka 2018/2019 hayakuweza kulipwa kwa wahusika na Jeshi halikufanya kazi kwa wahusika kutokana na asilimia 14.32 ya bajeti iliyotolewa. Tunaomba bajeti ya mwaka 2019/2020 kutolewa kwa ukamilifu ili maeneo ya Jeshi yatambulike na wananchi wasiwe na manung’uniko yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunasikitishwa sana na makazi ya wanajeshi wetu hapa nchini na kazi yao ngumu waifanyao na hawana muda maalum wa kazi yaani wapo mchana na usiku.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo tukiona bajeti ya Fungu 57 inatolewa kwa 1.47% ya mwaka 2018/2019 hadi sasa inasikitisha kwani dalili hii haioneshi kama tuna nia njema ya kuboresha makazi ya wanajeshi tukimuunga mkono Raisi wetu. Tunaomba pesa ya Fungu 57 itolewe kwa nia njema kwa asilimia kubwa zaidi tuwatolee tatizo hili la mazingira mabovu ya makazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja.