Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia Wizara hii ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, kulingana na umuhimu wa Wizara hii na mambo ya ugaidi yanayoendelea nchini na duniani kote, nitakwenda kuchangia mambo kadhaa ili kushauri Wizara hii ambayo ni muhimu kwa nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha zinazoidhinishwa na Bunge zipelekwe na kutolewa kwa wakati, naishauri Serikali kuzingatia maazimio ya Bunge ili kuleta ufanisi kwa Jeshi letu pia ufanisi wa utendaji kazi wa Jeshi lenyewe na kwa Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu migogoro ya wanajeshi na wananchi, kumekuwa na malalamiko makubwa kutoka kwa wananchi hususani wale wanaozunguka maeneo ya Jeshi kunyang’anywa maeneo yao kwa nguvu na kuwatesa wananchi wanaozunguka maeneo ya Jeshi, hali sio nzuri wala haileti sura nzuri kwa Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, posho ya chakula kwa wanajeshi ni vyema Serikali kulipa jambo hili umuhimu mkubwa ili kuleta motisha kwa wanajeshi wetu na familia zao, kwani wanajeshi wakiwa na manung’uniko ni hatari kubwa hasa kwa kuangalia umuhimu wao katika masuala ya ulinzi wa Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pesa za mafunzo kwa wanajeshi kumekuwa na utaratibu mbaya sana kwa wanajeshi wa nchi yetu wanapotaka kujiendeleza kimasomo, wengi wao wanajitegemea wenyewe. Suala hili linaweza kuondoa utendaji bora, kwani pesa ambayo alitakiwa kusaidia familia zao ndiyo analipa masomo, inawakatisha tamaa wanaotaka kuendelea na masomo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu upandishwaji wa madaraja, kumekuwa na malalamiko kutoka kwa wanajeshi waliokidhi vigezo vya kupandishwa madaraja, nashauri Serikali kufuatilia jambo hili kwa busara kubwa na kumaliza tatizo hili ili kuleta motisha ya kazi kwa wanajeshi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanajeshi waliopata mafunzo na baadaye kuachwa mitaani bila kazi kuna athari kubwa sana kwani vijana hawa wanapewa baadhi ya mafunzo ambayo ni ya kijeshi ambayo kwa kubaki kwao mitaani inaweza kuwa hatari kubwa zaidi kwa nchi yetu, ni vyema Serikali ikabadilisha utaratibu ili kulinda nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali iwe inawaandalia kazi za kufanya baada ya kutoka kwenye mafunzo.