Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Nuru Awadh Bafadhili

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. NURU A. BAFADHILI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote napenda kumshukuru Mungu kwa kuniwezesha kuchangia hoja iliyopo mbele yetu. Mchango wangu nitajikita juu ya utendaji kazi wa wanajeshi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanajeshi wameonesha uadilifu katika utendaji kazi zao katika maeneo mbalimbali. Tukichukulia uadilifu na uharaka walioonesha katika ujenzi wa nyumba za wafanyakazi na ofisi za Mji Mpya wa Serikali, Dodoma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali haioni umuhimu wa kuwapa tender za ujenzi wa nyumba na ofisi za Serikali kutokana na ubora wa majengo yao wanayoyajenga na pia uharaka wa kuyakamilisha?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna vijana ambao wapo katika Kambi za JKT vikosi mbalimbali ambao wako tayari kutekeleza litakaloamrishwa. Je, kwa nini badala ya kuweka walinzi katika aidha Ofisi za Serikali, majumbani na nyumba za watu binafsi kuajiri walinzi ambao siyo waaminifu na wengine hawajulikani makazi yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwa nini tusitumie vijana wetu wa JKT kufanya kazi hizo ili kuinua vipato vyao na pia Serikali kupata fedha? Mfano hawa Security Groups wanapolinda aidha nyumbani wanadai shilingi 300,000 kwa mwezi, yule mlinzi analipwa shilingi 60,000, sasa hii inapelekea mlinzi kutokuwa mwadilifu katika kazi yake. JKT wakipewa hii tender watalinda kwa uadilifu na vilevile mfano hizo shilingi 300,000 anaweza akapewa mlinzi shilingi 150,000 na 150,000 ikaingia katika mfuko wa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho ni kuhusu wanajeshi wetu, wanajeshi hawa wanaendelea kuonesha uaminifu wao kwa nchi na Serikali kwa ujumla. Basi Serikali ione umuhimu wa kuwapa stahili zao vilevile na upandishwaji wa vyeo. Hawa ni watu muhimu katika ulinzi wa amani ya nchi yetu, lazima tuwathamini na kuonesha umuhimu wa Serikali kwao, tusiwakatishe tamaa. Ninamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutupa nchi ya amani na utulivu wakati kuna nchi nyingine tuko jirani nazo hawalali wala kufanya kazi kwa amani kutokana na vurugu za mara kwa mara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuwaenzi wanajeshi wetu na tuwathamini kwa kazi zao nzito wanazofanya.