Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. SUZANA C. MGONUKULIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na uzito wa Wizara ya Ulinzi, Serikali itoe fedha za maendeleo zilizoidhinishwa kwa ajili ya Fungu 38 kwa mwaka wa fedha 2018/2019 ili kuhakikisha shughuli zote zilizopangwa na Wizara hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, amani tunayoiona hapa nchini ni kwa sababu mipaka yetu inalindwa vizuri, kwa kutotoa fedha za maendeleo kutasababisha Wizara hii isitimize wajibu wake kiurahisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeshindwa kulipa fidia kwa wananchi kwa maeneo yaliyochukuliwa na JWTZ na JKT na kutoa muda mrefu bila kulipa fidia jambo ambalo licha ya ucheleweshaji haki hadi wamiliki wameshafariki na hivyo kudhulumika. Ifike wakati Serikali isiwanyanyase wananchi kwa kiasi hicho. Kwa maeneo yote ambayo hadi leo fidia haijalipwa basi kwa bajeti ya mwaka 2019/2020 ilipe fidia zote.