Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami kwa namna ya pekee nashukuru kwa kunipa nafasi hii. Naomba kwanza nianze kwa kukupa hongera nyingi sana Profesa Ndalichako na timu yako, mnafanya kazi nzuri, hongereni sana. Hiyo ni tafsiri kabisa kwamba akina mama wenye ujuzi, mnaweza, hongereni sana! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wizara hii, niseme tu kwamba Mheshimiwa Waziri unafahamu kwamba asilimia 68 ya Civil Service ya nchi hii ni Walimu. Kwa hiyo, zaidi ya Watumishi wa Serikali hii ni Walimu. 68 percent ndiyo Civil Service ya nchi hii. Tafadhali sana! Wewe Mheshimiwa Waziri, Waziri wa TAMISEMI, Waziri wa Utumishi, kaeni pamoja kuhakikisha kwamba Walimu hawa tunawapa kipaumbele cha kwanza. Bila wao hakuna nchi hii. Sisi wote tuko hapa kwa sababu tulisoma, kwa sababu tulifundishwa na Walimu hawa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bila shaka kila mmoja anafahamu kwamba Walimu hawa wana changamoto nyingi sana. Shule zetu nyingi hazina nyumba za Walimu, shule nyingi hazina madarasa ya kutosha, Halmashauri zetu zinahangaika kushoto na kulia. Naomba, wakati umefika, Serikali yenyewe itafute fedha popote itakapopata fedha hizo, kujumuika na Halmashauri zetu ili miundombinu ya elimu iweze kuwa rafiki na hakika shule zetu ziweze kuboreka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, ambalo napenda kulisema, ni hili jambo la ada elekezi. Mimi huwa sielewi vizuri, labda Mheshimiwa Waziri atanifafanulia. Hivi ada elekezi ambazo mng‟ang‟ana na hao wenye shule, hizi shule siyo mali ya Serikali! Hizi shule ni mali ya watu binafsi. Mmekaa nao? Mmezungumza nao? Mmelewana? Maana yake haya ni kama mtu mwenye mali yako, halafu anakuja mtu mwingine anasema basi weka ada elekezi. Kila mmoja anajua nchi hii, miaka ya 1980 na 1990, watoto wetu walikuwa wakienda Kenya, Uganda na Malawi kusoma. Sasa wenye mitaji yao wameanzisha shule hizi, tunaanza kuja na ada elekezi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu na ushauri wangu kwa Serikali, kaeni na wamiliki wa shule hizi, ni mali zao, mwasikililize, Serikali ifanye facilitation tu. Hakuna sababu ya kugombana na hawa watu. Tunataka watoto wetu wakasome tena Kenya? Wakasome Uganda? Ni muhimu sana ada elekezi hizi mkubaliane na wamiliki wa shule, zile shule ni mali yao na kamwe siyo mali ya Serikali; na tumeshatoka huko ambako mali zilikuwa za Serikali, shule zilikuwa za Serikali; sasa shuke hizi ni za watu binafsi. Naomba sana jambo hili Mheshimiwa Waziri, wewe ni mahiri, wewe mwenyewe ni Mwalimu, mkae mliangalie vizuri mkubaliane na hawa wamiliki wa shule na muafaka upatikane.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina hakika mkizungumza na wamiliki wa shule, wana uelewa, wamewekeza fedha zao nina hakika mtafika mahali kwenye middle ground ambapo hata kama ni ada elekezi basi ni rafiki kwa wamiliki wa shule na kwamba pia watafanya biashara pamoja na kwamba elimu kwa kweli kwa kiwango kikubwa ni huduma zaidi kuliko biashara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo napenda niliseme ni haya mafao na malipo ya Walimu, kwa mfano, Walimu katika Halmashauri ya Mji wa Kasulu, Walimu katika Mkoa wa Kigoma, wamekuwa na malimbikizo mengi sana. Nimepata taarifa kwamba juzi wamelipwa, eti madai yao fedha iliyohakikiwa wameletewa asilimia 13 tu basi. Sasa anayefanya uhakiki ni nani huyo? Hawa Walimu ni kipaumbele. Naomba sana Walimu wa Halmashauri ya Mji wa Kasulu, Walimu wa Kasulu Mjini na Halmashauri wahakikiwe vizuri. Unafanyaje uhakiki unakuja na ten percent ya uhakiki! Ni kitu ambacho hakikubaliki. Ingekuwa angalau 40 percent, 50 percent unaweza ukaelewa, ten percent, 13 percent ya madai yao yaliyohakikiwa, hilo ni dhahiri kabisa kwamba kuna mahali kuna tatizo na tatizo tusiliruhusu likachafua Serikali ya Awamu ya Tano ambayo imeanza kwa matumaini makubwa kwa Watanzania hawa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo napenda nilizungumze, sisi Mkoa wa Kigoma, tumeanza kujenga a grand High School, Shule ya Sayansi. Maana yake Waheshimiwa Wabunge mnafahamu kwamba Mwanasayansi aliyepata tuzo ya Nobel katika nchi hii, anatoka Mkoa wa Kigoma. Tumeanza kwa juhudi zetu wenyewe, tumejenga a ground high school, shule ya sayansi. Imejengwa pale Kasulu, tumejichangisha wenyewe, mkoa mzima tumepata karibu shilingi milioni 600 na tumeanza kujenga shule pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba sana Wizara nayo, wewe Mheshimiwa Mama Ndalichako ni mdau, nawe kama Wizara na Serikali kwa ujumla mwangalie namna nzuri ya kusaidia juhudi za watu wa Kasulu na watu wa Kigoma ili hatimaye ile grand high school baadaye tuibadilishe iwe Chuo Kikuu. Kitakuwa Chuo Kikuu cha kwanza cha sayansi. Nina hakika kwa uwezo wa vijana wa Kigoma, kitatoa wanasayansi walio bora na walio mahiri sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi hiyo imeshaanza na wenzetu wa SUMA JKT wametupa ushirikiano mzuri sana, ndio wanatujengea eneo hili. Nasi Halmashauri ya Mji wa Kasulu tumetoa eneo bila fidia, eneo la ekari 115 nami Mbunge wao nimetumia kila lililokuwa ndani ya uwezo wangu, kuhakikisha kwamba eneo lile limepimwa na linamilikiwa kihalali sasa na Halmashauri na Mkoa wa Kigoma kwa ajili ya ujenzi wa Grand High School. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho nizungumzie ujenzi wa makitaba. Sisi pale katika Mji wa Kasulu tumejenga maktaba. Kipindi kile nikiwa Mbunge mwaka 2005 tulijenga maktaba kwa kushirikiana na wenzetu wa Tanzania National Parks. Tumejenga jingo kubwa, lina gorofa mbili. Jengo lile limegota, nafikiri ni wakati muafaka umefika sasa Wizara na Serikali mwingilie kati mtupe nguvu, mtusaidie ili jengo lile sasa lianze kufanya kazi. Malengo na madhumuni ni kufanya maktaba ile kiwe ni kituo cha elimu katika Mji wa Kasulu na ni mji ambao unakua kwa haraka sana kama miji mingine inavyokua katika nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, naomba nizungumzie suala la ukaguzi wa shule. Mheshimiwa Waziri, shule hazikaguliwi. Waheshimiwa Wabunge shule za Sekondri na za Msingi hazikaguliwi. Sasa shule hazikugaliwi…
MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana, naunga mkono hoja hii, ahsante sana.