Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Salum Mwinyi Rehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nichukue fursa hii kukushuruku kwa kupata nafasi ya kuchangia katika Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka kuzungumza mambo mtatu ambayo zaidi ni kushauri katika Jeshi letu hili na hasa kwenye upande wa JKT. JKT kwa sasa tunaweza kusema kwamba ni moja kati tegemeo na nguzo mahiri kabisa ambayo inaweza kututolea vijana ambao wanaweza kushiriki harakati mbalimbali Jeshi wa Taifa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kubwa zaidi tunachotaka hapa ni kuweza kutolewa mafunzo yale ya ueledi zaidi katika Jeshi letu hili la JKT na hasa yale ya kuwafanya vijana wale wakitoka pale waende wakajitegemee. Pamoja na mafunzo yanayotoka sasa hivi, lakini bado hayawajengi wale vijana na kuwapa ile confidence ya kumaliza JKT na kuweze kwenda kujitegemea na wengi wao wanakwenda kwa mawazo kwamba hawapati ajira kitu ambacho Serikali haiwezi ku-afford kuwapa ajira watu wote ambao wanaweza kwenda katika maeneo haya ya JKT.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo wito wangu kwa nini kusianzishwe programu maalum ndani ya JKT ambazo zitawafanya vijana wale waweze kuwa mahiri hasa kwenye upande wa kilimo, mifugo na uvuvi. Tuna mahitaji mengi vitu sasa hivi katika nchi yetu lakini tuna matishio ya hali mbalimbali za hali ya hewa ambazo zinakabiri mazingira yetu kama tungeweza kuliimarisha Jeshi hili la JKT hasa kwa kuzalisha kwenye kilimo cha umwagiliaji maji wakaweza kuzalisha mazao mengi kabisa hasa na tatizo hili la upungufu wa chakula au tishio la ukame ambalo linatokea katika maeneo yetu mbalimbali tungeweza kulikabili na hii ingekuwa ni sehemu moja ya kuwa na food reserve kuliko hali inavyokwenda sasa hivi. (Makofi)

Kwa hiyo, wito wangu zaidi ni kulitaka jeshi hili lijitengeneze upya na kuweza kujitegemea hasa kwa ajili ya chakula na mimi maoni yangu binafsi ningependelea wangeweze kuwa kama walivoambiwa Magereza na wao JKT waweze kujitegemea kwa chakula na sio Serikali iweze kuwalisha siku zote wakiwa makambini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine katika eneo hili ningeomba JKT kupitia Shirika lake lile SUMA na mashirika mengine yaliyoko katika Jeshi la Kujenga Taifa, Jeshi la Wananchi kuweza kujenga ile bandari ya uvuvi. Jeshi limeweze kulipa eneo lile Ras Mshindo, eneo ambalo ni sahihi kabisa kwa ajili ya kujega bandari ya uvuvi. Bandari ile haitaumika kwa sababu ya uvuvi lakini itatumika kama ni sehemu ya karakana meli mbalimbali ambazo zitakuwepo pale ziwe za kijeshi, ziwe za wananchi, ziwe za nje, za sehemu nyingine mbalimbali ambazo zitatengeneza mazingira mazuri ya fedha na kulifanya Jeshi kuwa na mitaji na miradi ya mikakati zaidi kuliko hali inavyokwenda hapa.

Lakini vilevile itadaia katika eneo lile kuweza kulinda mazingira sasa ya bahari kuliko sasa hivi maeneo yetu ya bahari umekuwa ni mkubwa, lakini Wizara inayohusika na taasisi nyinginezo hazina doria wala udhibiti wowote wa mazingira ya bahari tunalitegemea jeshi hili liweze kuzunguka katika maeneo yetu ya bahari yaweze kuyalinda, lakini kudhibiti uchafunzi ambao unafanyika hasa sasa hivi ulioingia utupaji wa takataka za kemikali katika bahari zetu na maeneo yetu mbalimbali ya uzalishaji. Kwa hiyo, ningeomba zaidi Jeshi hili lingejikita katika mwelekeo huo na kuweza kujiimarisha zaidi katika maeneo yetu ya bahari ambayo yana fursa kubwa zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ambalo nilitaka nilizungumze ni suala zima ya kuimarisha vikosi vyetu hasa kwenye mambo ya michezo kuna fursa kubwa kupitia Jeshi hili la JKT na Jeshi la Wananchi kuimarisha michezo kama ilivyokuwa zamani inavyoonekana sasa hivi ule mwendelezo hasa na makakati uliokuwepo umepungua nguvu. Kwa hiyo, nimkumbushe Waziri lakini nimkumbeshe CDF na wenzake ya kuweza kuimarisha michezo na kulifanya Jeshi kuonekana kwamba ndio ramani sasa ya michezo Tanzania kama wanavyotumia wenzetu kwa sababu ukiangalia Marekani, Uingereza na maeneo mengine wanajeshi ndio wanakuwa wameshika hatamu hasa michezo na inakuwa ndio dira na nembo ya Taifa zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningemuomba CDF kuangalia mbinu na njia gani ya kuimarisha sekta hii ya michezo katika Jeshi ambavyo inaweza kutusaidia kuwafanya wanajeshi wetu kuwa mahiri lakini vilevile na kutunza afya zao kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hayo nakushuru sana. (Makofi)