Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nimshukuru Mwenyenzi Mungu kwa kunitete na nikiwa kwenye swaumu Ramadhani naendelea salama nimshukuru Mungu. Awali ya yote Mwenyezi Mungu nimuombe aniongoze niongee kauli ambayo itampendaza Mwenyezi Mungu na itapendeza Tanzania kwa ujumla. Niipongeze kwanza Kambi ya Upinzani kwa hotuba waliyoiwasilisha na haya waliyoyatoa namuomba kaka yangu Mheshmiwa Waziri ni mweledi, ni mwerevu na makini, ayachukue na ayafanyie kazi katika Wizara yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitajikita kwanza kauli zinazotolewa na Wakuu wa Majeshi tuangalie, kauli yoyote inayotolewa na Mkuu wa Jeshi ni kauli wananchi, ni kauli ambayo inatakiwa iwe ni kauli ambayo haina ukakasi, iwe ni weledi kwa sababu mwaka 1978 ilikuwa ikitolewa kauli kwenye Jeshi, wananchi wote wanasimama, wanatulia, wanasikiliza kauli hii ina kitu gani. Lakini sasa hivi tumeona Jeshi letu linaanza kutanatoa kauli ambazo zina ukakasi, kwa hiyo, nimuombe Mkuu wa Majeshi awe mweledi kwa kutoa kauli ambazo zitaenda na Taifa letu na Tanzania kwa ujumla bila ya kuuingiza siasa ndani yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo kuna wanajeshi wachache wanaochafua jeshi, wanaingia mitaani wakunywa pombe za watu, wanavunjwa vitu vya watu, hawalipi pesa, wengine wanawapa wanawake mimba hawawashughulikii wanawake, hawawapi mahitaji na hata wanavyokwenda kutaka mahitaji yao wanakutana na Wakuu wa Majeshi kwa hiyo sasa inakuwa tunaongeza watoto wa mitaani. Kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Waziri alifuatilie kwa kina maaskari wote wanajeshi wanapowapa wanawake mimba basi wanawake hawa wapate stahiki zao na walelewe watoto, tutoe punguzo la watoto wa mitaani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine tulikuwa na kiwanda chetu tulikuwa tunaona wanajeshi wananunua viatu kutoka Bora walikuwa wanavaa viatu vizuri. Lakini sasa hivi viatu hivi vinatengenezwa China, havina umahiri wowote yaani buti likipigwa mara moja tu kiatu kinachanika. Sasa ni kwa nini hivi viwanda vya ndani visiimarike, vikatunzwa, vikatengewa bajeti ya kutosha vikatengeneza sare za wanajeshi na viatu vya wanajeshi. Kama Magereza na vinginevyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tukiangalia pia kwenye masuala ya makazi ya wanajeshi tumeona wamejitahidi kwa kweli wamejenga makazi ya wanajeshi. Lakini kwenye makazi ya wanajeshi tunaona kuna ubadhirifu uliotumika, ni kwa nini sasa wasitumie wakandarasi wa ndani angalau tungepata hata makazi bora na bora zaidi kuliko haya makazi haya yaliyojengwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine tuangalie migogoro ambayo inatokewa kwenye mipaka, maeneo ya Jeshi ambao wananchi wanayavamia niombe Jeshi wafanye uhakiki kwenye mipaka ya Jeshi ili hawa wananchi ambao wanasogea kwenye mipaka ya Jeshi na kujenga na kuanza kulima mazao kwa baadae wanavyokuja wananchi kuwabomolea wanajenga taswira mbaya na chuki kwa wananchi. Kwa hiyo, niliombe Jeshi pia wahakiki mipaka yote ya Jeshi na kuhakikisha wananchi ambao wamevamia maeneo ya Jeshi wanatolewa kwa utaratibu unao stahiki kama wengine wanalipwa stahiki zao pia waondoke sio kuharibu mazao ya wananchi, na pale labda wananchi wamelima vitu vile basi angalau wawape muda wakishavuna wawaambie basi waondoke sio kuwapiga. Kwa sababu wananchi wengi wategemea Jeshi la Wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine tuangalie wastaafu wa Jeshi pia hawajalipwa stahiki zao, wale ambao wanadai stahiki zao zilipwe kwa wakati hizi stahiki zilipwe za wanajeshi kwa sababu imekuwa siku nyingi sana wanavyomaliza basi wanachukua muda mrefu hawapewi stahiki zao.