Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru kwa nafasi, niipongeze hotuba ya Kambi ya Rasmi ya Upinzani Bungeni wamesema dhahiri kwamba Jeshi lifanye kazi ya kulinda mipaka ya nchi na ninarudia Jeshi letu tunalipenda sana liendelee kupambana tunapongeza uzalendo wao watulinde. Mambo ya ndani ya nchi kwa maana mambo ya siasa tuwaachie wanasiasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina hoja mbili kwa sababu ya muda, changamoto ya bima ya afya kwa wanajeshi; natambua kwamba wanajeshi wanatibiwa na wanaambiwa watimbiwe kwenye Hospitali ya Jeshi, lakini changamoto inatokea kwamba si kila sehemu ya nchi hii kuna Hospitali ya Jeshi. Wanaopaswa kutibiwa wakati mwingine ni wazazi wa mwanajeshi, ni mwenza wa mwanajeshi na watoto na sio lazima wote wawe wanaishi kwenye eneo la kambi. Nadhani Wizara iangalie na iipe kipaumbele kama ambavyo sisi tunatibiwa na bima za afya na kuchagua ni wapi pa kupata matibabu basi na wananajeshi wazalendo wanaopigania nchi hii wapate haki hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili nitaongelea Fungu Namba 39 ambalo ni JKT natambua JKT kwamba inafanya biashara kwa kupitia Shirika lake la SUMA JKT. Lakini kumekuwa na changamoto kubwa sana kwenye SUMA JKT kiasi kwamba wakati mwingine nakuwa napata wasiwasi CDF wanavyokuwa wa busy anafanyakazi au awaza kufanya kazi ya IGP huku SUMA JKT mbona mambo hayaendi sawa? [Maneno Haya Siyo Sehemu ya Taarifa Rasmi za Bunge]

Mheshimiwa Mwenyekiti, SUMA JKT wamekuwa wanajiingiza kwenye mikataba ambayo si tu haina tija kwa Taifa lakini inahatarisha hata uhai au afya ya usalama wa ndani ya nchi yetu mfano SUMA JKT waliingia mkataba na Shirika/Kampuni ya Kichina la Holley ambayo baadae ikaja kuitwa Tanzansino mwaka 2016. Walitaka kuingia kwenye biashara ya kuzalisha madawa mkataba ukavunjika, lakini sehemu ya ubia ya mkataba ilikuwa ni ardhi ya jeshi, makubliano yakawa katika kuvunja mkataba na ile sehemu ya jeshi ikatolewe ardhi ikatolewa kati China na Tanzania. Walilazimika kutoa fedha kwa ajili ya kunusuru ardhi ya jeshi, you can imagine watu wanaingia mkataba mpaka kukubali eneo ya jeshi liwe sehemu ya makubaliano ya lile eneo ni hatari sana kwa mustakabali wa uhuru wa nchi yetu au mambo ya ndani ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili hawa hawa SUMA JKT waliingia mkataba na Cami katika kiwanda chao cha uzalishaji nguo kinaitwa Cami Suma. Cami Suma walipaswa kuzalisha nguo, walilenga kulisha Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla. Mkataba umevunjika, hakuna kilichoendelea, lakini kinachosikitisha kati ya Tanzansino na Cami Suma waliendelea kutoa fedha zaidi ya milioni kumi kwa ajili ya ku-service zile mashine, lakini pia na umeme. Unaona kwamba wanaingia kwenye mikataba mibovu, fedha zinatumika na hakuna tija inayopatikana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sio huo tu mkataba waliingia pia SUMA JKT na shirika moja linaitwa Equator Automatic Company ambayo hii nayo ni ya China, lengo lao lilikuwa kuunganisha magari makubwa, magari ya fire, vifaa vikubwa kwa ajili ya ujenzi mkataba huo huo ukasuasua. Mkataba sasa hivi upo kwenye wind up, wakaingia kwenye mkataba mwingine na Kampuni ya Kichina inaitwa Chenggong Limited huo mkataba ambao ni wakuingiza mashine kubwa kubwa kwa ajili ya ujenzi, kukodisha lakini pia na kuuza. Mpaka naongea hapa kumekuwa nakusuasua kwa vibali kwa sababu wakati mwingine mashine zinazoingizwa nchini ni kubwa. Huo ni mfano mdogo tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, SUMA JKT ambayo inauza haya matrekta ambayo yote tunayajua ali maalufu kama SUMA iliingia mkataba na Kampuni ya URSUS SA kutoka Poland ikiwa ni mkataba wa zaidi ya bilioni 119. Huo mkataba wenyewe masharti hayakutimia mpaka tunavyoongea leo masharti hayakutimia kuna baadhi ya mashine hazikuja na tunavyoongea leo humu ndani kuna zaidi ya Wabunge wanadaiwa milioni 500 hawajalipa, watumishi wa umma wanadaiwa zaidi ya bilioni moja hawajalipa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ninajiuliza hiyo SUMA JKT ipo kwa ajili ya kusaidia Taifa kwa kupitia biashara au ipo kwa ajili ya kuangamiza Taifa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, na badala namshauri CDF ajikite katika kusaidia hizi taasisi, kwa mujbu wa CAG taarifa ya 2015/2016 kumekuwepo na zaidi ya bilioni 1.14 zimetumika bila kufuata matumizi ya manunuzi ikiwa ni pamoja na bila kupita kwenye Bodi ya Wakurugenzi. Kuna changamoto kumbwa sana ambayo kama Jeshi tunalolitegemea litulize...

MWENYEKITI: Ahsante.