Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Gimbi Dotto Masaba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. GIMBI D. MASABA: Mheshimiwa Naibu Spika, mnamo tarehe 27 Kamati ya Viwanda ilikutana na wafanyabiashara wa makampuni kama zaidi ya 23. Katika kikao hicho, changamoto za mlundikano wa kodi zilitawala sana ila naomba nibebe haya machache kuhusiana na viwanda vya ndani vya kuyeyusha chuma.

Mheshimiwa Naibu Spika, uwekezaji wa viwanda 16 vya chuma nchini ni dola milioni 170.3 ambayo ni takribani shilingi bilioni 392 na vinatoa ajira kwa Watanzania 25,913. Uwezo wa viwanda hivi kuzalisha kwa mwaka ni tani 1,082,700. Uzalishaji wa sasa ni tani 240,336 sawa na 22% tu na shida kubwa imeelezwa ni uhaba wa chuma nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, akiba ya chuma tuliyonayo kama nchi ni tani milioni 126 ambazo zinaweza kuchimbwa metric ton milioni tatu kwa zaidi ya miaka 100 ambapo uhitaji wa chuma wa Taifa ni metric ton 440,336 ukiondoa chuma kwa ajili ya SGR ambapo hata nati moja inatoka Uturuki ambapo Afrika Mashariki pekee kwa mwaka inaingiza chuma chenye thamani ya dola bilioni 1.5 sawa na trilioni 3.3 thamani ya kiwanda cha makaa ya mawe na chuma cha Liganga na Mchuchuma ni dola bilioni 2.9 sawa na shilingi trilioni 6.38 fedha ambayo tunairudisha kwa miaka miwili tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania kwa mwaka inaingiza chuma zaidi ya metric ton 200,000 sawa na 45% tu mahitaji ya chuma. Tena chuma hiki kinaingizwa kwa kodi kidogo au bila kodi kabisa huku tukijua tunadhoofisha sana viwanda vingi kujiandaa kufungwa. Hivyo, naomba kodi ya dola 400 kwa metric ton iongezwe ili kufidia gap kwa wafanyabiashara wa ndani.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba mambo matatu kwa Waziri wa Viwanda na Biashara. Naomba chuma kinachotoka nje kiongezwe ushuru hadi kufikia dola 400 kwa metric ton ili kulinda viwanda vya ndani. Kwa nini tunashindwa kuanzisha kiwanda chetu kwa ajili ya kuyeyusha chuma hapa nchini ili hata SGR ijengwe kwa chuma chetu?

Mheshimiwa Naibu Spika, ile kampuni SHGL iliyokuwa inataka kununua migodi ya Liganga na Mchuchuma kwa miaka 100 ili wao wachukuwe 80% na Tanzania 20% makubaliano yamefikia wapi? Naomba kufahamu kuhusu wafanyabiashara kumi wa mji wa Kahama ambao walikamatwa toka mwezi wa 10 mwaka 2018 mpaka leo wana miezi saba wako ndani na hawajui hatima yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba Mheshimiwa Waziri afike katika Gereza la Shinyanga Mjini kujua hatima ya wafanyabiashara hao. Nini hatima yao? Naomba kama wamebainika na kosa wapigwe faini na waachwe waendelee na biashara zao. Ili kuweza kufikia uchumi wa viwanda ni lazima wafanyabiashara wetu tuwaone kwa jicho la huruma zaidi, kwani ndio nguzo ya Taifa letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.