Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. SUZANA C. MGONUKULIMA: Mheshimiwa Naibu Spika,, Mradi wa Liganga ni miongoni mwa miradi ya kimkakati na ulianzishwa kwa lengo la kujenga kiwanda cha kufua chuma. Utekelezaji wa mradi huu umechukua muda mrefu, takribani miaka nane bado haujaanza. Kamati ilijulishwa na Wizara juu ya tathmini waliyoifanya katika bidhaa za chuma na kubaini kuwa vinakumbana na changamoto ya upatikanaji wa malighafi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa nia ya Serikali ya nchi yetu ya Tanzania ni kuwa nchi ya viwanda, kuna kila sababu kwa Serikali kuhakikisha inajipanga kukamilisha mradi huu wa Liganga ili chuma kinachopatikana iwe malighafi ya viwanda vyetu hapa nchini. Kwa kufanya hivyo, mapato yataongezeka na hivyo basi, tutakuza uchumi wa Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili tufikie malengo ya nchi yetu ya viwanda, Sekta ya Kilimo lazima iboreshwe. Hakuna viwanda bila kilimo. Hadi sasa Sekta ya Kilimo imesahaulika kabisa, pembejeo hazipunguzwi ruzuku ili wakulima wote wapate pembejeo na kwa kuwa asilimia 75 ya Watanzania ni wakulima.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na utoaji wa vitambulisho kwa wajasiriamali kwa utaratibu mpya, Serikali inapoteza mapato. Mjasiriamali ambaye alikuwa analipa ada/ushuru wa shilingi 500/= kwa siku kulingana na biashara yake, itamlazimu kwa mwezi kulipa shilingi 15/= ukizidisha kwa miezi 12 sawasawa na mwaka mmoja mjasiriamali huyu atalipa jumla ya shilingi 180,000/=. Kitambulisho hiki kinatozwa shilingi 20,000/=.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hesabu ya kawaida 180,000 – 20,000 = 160,000. Ukichukua wafanyabiashara wadogo wadogo, wapo wengi sana hivyo kwa kutumia njia hiyo Serikali inapoteza mapato makubwa sana. Serikali ijitathmini kuendelea na mpango huu au kubadilisha ili Serikali iendelee kupata mapato kutokana na tozo za mauzo ya ujasiriamali.