Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, service levy imekuwa kero kwa wafanyabiashara iondoshwe haraka, hakuna mkakati mkubwa wa kusaidia kilimo kwa lengo la kufungamanisha uchumi wa viwanda na kilimo.

Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto ya umeme inaendelea kuwepo kwani, kuna kupungua na kuongezeka umeme hasa eneo la Ukanda wa Pwani kiasi cha kuathiri viwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, chuma cha Liganga na Mchuchuma, ndiyo namna pekee ya kuendeleza mradi wa SGR, vinginevyo tutapoteza fedha nyingi kununua chuma, kutoka Japan, Serikali iangalie na kuufanya mradi huu wa kipaumbele kati ya vipaumbele vingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutekelezwa Mradi wa Bagamoyo wa SEZ; Serikali lazima ije na kauli moja juu ya hatma ya Mradi wa Bandari ya Bagamoyo, Serikali lazima ione economic impact ya kuanzisha mradi huu mkubwa kwa Taifa. Ni rai yangu Serikali ijifunze na kupembua ni ipi miradi ya mkakati na ianze nayo badala ya miradi mingine, ambayo tija yake inategemea miradi mingine, mfano SGR, inategemea ufanisi wa bandari.

Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto ya korosho ni rai yetu kuwa wakulima wote watatendewa haki katika kwa malipo stahiki ya mazao yao. Aidha, natoa rai kwa Serikali kuendelea na kuhakikisha mambo haya hayajitokezi tena.

Mheshimiwa Naibu Spika, Sera ya Nchi ya Uchumi wa Viwanda; haiko clear, ni rai yangu Wizara itakamilisha suala hili haraka. Sera hii ijibu masuala ya PPP mazingira ya kufanyia biashara, elimu za biashara na kadhalika.