Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Naibu Spika, nipende kuchukua nafasi hii kuchangia Wizara ya Viwanda na Biashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna eneo la ardhi ya wananchi ambao wametoa ardhi yao kwa EPZ ambao wamechukua eneo la Kata ya Mwengemshindo katika Manispaa ya Songea, lakini wananchi hao hawajalipwa fedha zao za fidia mpaka sasa. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha wananchi hawa ambao wamekuwa wakisubiri kwa muda mrefu bila kulipwa fedha, walipwe ili waweze kuendeleza shughuli zao?

Mheshimiwa Naibu Spika, Kiwanda cha Usindikaji wa Tumbaku (SONAMCU) kilichopo katika Manispaa ya Songea, mwaka jana mwezi Mei niliuliza ni lini Kiwanda cha SONAMCU kitaanza, majibu yalikuwa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeshapata mwekezaji ambaye tayari ameshasaini mkataba wa kuendesha kiwanda hicho na kwamba kiwanda hicho kitaanza kufanya kazi Mwezi Agosti, 2018, lakini mpaka sasa kiwanda hiki hakijaanza; tatizo ni nini?

Mheshimiwa Naibu Spika, tangawizi; katika Wilaya ya Songea Vijijini katika Kata ya Mkongotema, Wino, Madaba na Maweso wanalima sana zao la tangawizi ambalo limekuwa linatumika kama chakula, dawa na kadhalika. Kwa kuwa zao hili ni muhimu sana na linazalishwa kwa wingi katika maeneo niliyoyataja, Wizara hii ingetafuta namna ya kufanya au kuwasaidia wakulima hao kupata wawekezaji wa kiwanda ili waweze kuongeza thamani ya zao hili na tija kwa maisha yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara iangalie namna ya kuwawezesha wakulima wa zao la mahindi kwa kutafuta wawekezaji wa viwanda vya uchakataji wa zao la mahindi. Ni matumaini yangu kuwa Wizara ikijipanga vizuri haya yote yanawezekana.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba mchango wangu huu wote uingie kwenye Hansard.