Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa fursa hii. Nianze kwa kumpongeza Mtoa Hoja Mheshimiwa Waziri Joseph Kakunda kwa wasilisho zuri asubuhi ya leo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kisiwa cha Mafia kimejaaliwa hazina kubwa ya rasilimali za bahari na aina mbalimbali ya samaki. Kwa sasa kuna kiwanda kimoja tu cha kusindika samaki, naishauri Serikali yangu makini kuangalia uwezekano wa kujenga kiwanda kikubwa cha kusindika samaki katika Wilaya ya Mafia.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni kiwanda cha kusindika nazi; Tanzania inaongoza katika Afrika katika kulima nazi na inashika nafasi za juu katika dunia. Kisiwa cha Mafia kinalima zao hili kwa wingi lakini hadi sasa hakuna kiwanda hata kimoja cha kusindika nazi na mazao yanayotokana na nazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni utendaji kazi wa Shirika la Viwango (TBS);ni ukweli usio na shaka TBS inakabiliwa na changamoto kubwa ya vifaa vya kupima ubora ili iendane na kasi ya ukuaji wa viwanda nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni mfumo wa malipo ya ushuru wa bidhaa kwa kielektroniki yaani ETS; ni ukweli usio na shaka mfumo huu umesaidia kuongeza mapato ya Serikali, ni ushauri wangu sasa Serikali iongeze wigo wa bidhaa zinazotumia mfumo huu katika vinywaji na sigara kwenda kwenye bidhaa nyingine kama cement, nondo na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na naunga mkono hoja.