Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Joyce John Mukya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. JOYCE J. MUKYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kuna uhusiano mkubwa kati ya sekta ya kilimo na ukuaji wa uchumi wa viwanda. Kama inavyoeleweka vision ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuendeleza viwanda nchini na kukuza uchumi wa kati kupita viwanda hivyo, lakini ili viwanda viweze kuzalisha kwa kiwango ambacho kitazalisha vizuri na kukuza uchumi wa kati, tunahitaji material, human resource na haya kwangu ni mambo muhimu zaidi kwa viwanda vya ndani. Sasa kama tunavyofahamu kilimo sasa hivi hapa Tanzania hakipovizuri kutokana na hali ya uchumi wa wananchi kuwa chini kwa kushindwa kuhudumia mazao yao ipasavyo kutokana na huduma za pembejeo, mbegu, kuwa juu na vilevile hali ya hewa kwa sasa siyo nzuri sana kwa wastani wa mazao ya wakulima kilimo kinachangia takribani 65% ya malighafi zote za viwandani.

Mheshimiwa Naibu Spika, napendekeza Serikali ihakikishe inaboresha kwanza kilimo na kuelekeza katika viwanda ambavyo vitaongeza thamani katika uzalishaji wa mazao mbalimbali. Mfano ya mifugo kama ngozi, maziwa, kwato, pembe, damu, ambavyo vyote hivi vinasaidia katika kutengeneza bidhaa mbalimbali kwenye viwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, manyanyaso ya wafanyabiashara mbalimbali tokea Awamu ya Tano imeingia madarakani; kumekuwa na matatizo makubwa kwa wafanyabiashara nchini kama vile hawana uhalali wa kufanya biashara au kutafuta njia mbadala ya kujikimu katika maisha kama sekta nyingine zinavyofanya. Wafanyabiashara ndiyo walipakodi wakubwa katika nchi hii, lakini wamekuwa hawatendewi haki kabisa na biashara sasa hivi imekuwa ni kama kansa katika nchi yetu. Kodi zimekuwa nyingi zaidi ya 25 ili tu kuanzisha kampuni yoyote ya kibiashara nchini. Hili linafukuza hata investors ambao wanataka kuja nchini kuwekeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuishauri Serikali kuwasaidia wafanyabiashara katika kuhakikisha wanakua na mazingira mazuri ya kufanya biashara na kuisaidia Serikali pia hata kufanikiwa katika kupata kodi kupitia biashara wanayofanya, lakini pia wafanyabiashara wanasaidia sana katika kuendeleza uchumi wa kati kupitia viwanda ambavyo ni vision ya Serikali ya Awamu ya Tano.