Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuchangia Wizara ya Viwanda na Biashara, Wizara ambayo ni muhimu kwa uchumi wa nchi yetu kwa kuzingatia mambo muhimu ili kufikia uchumi wa kati.

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa kiwanda cha mbolea; kulingana na umuhimu wa kilimo katika kukuza viwanda au uchumi ni vyema kutazama hitaji kubwa la bei kubwa ya mbolea; ili kumaliza tatizo hilo tujenge kiwanda cha urea.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la wafanyabiashara kufunga biashara zao; kumekuwa na mabadiliko makubwa kutoka kwa wafanyabiashara badala ya kuongeza wafanyabiashara inakuwa kinyume chake. Nashauri Serikali kufuatilia suala hili ili kuendelea kuinua uchumi wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Maafisa wapewe elimu pamoja na malalamiko mengi ya wafanyabiashara wengi nchini kwenye halmashauri zetu, lakini huko kuna Maafisa Biashara inaonekana wafanyabiashara sasa hawaoni umuhimu wa Maafisa hawa kwani miongoni mwa majukumu ni pamoja na kutoa elimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, bei ya sukari kuendelea kupanda; Wizara ina mkakati gani wa kuweza kudhibiti bei ya sukari kwani suala hili linaathiri kwa kiasi kikubwa wananchi wa hali ya chini. Pia nataka kujua kununua sukari nje ya nchi kunapunguza bei ya sukari au inaongeza bei kwa nini?

Mheshimiwa Naibu Spika, kodi ya huduma; suala hili limekuwa na changamoto kubwa kwa wafanyabiashara pia lina wafanya wafanyabiashara wetu kukata tamaa na wengine kuhama. Nashauri Serikali kuleta marekebisho ya sheria hiyo ndani ya Bunge letu ili ifanyiwe marekebisho.

Mheshimiwa Naibu Spika, mazingira ya biashara yasiyotabirika; kumekuwa na shida kubwa kwa taasisi mbalimbali zinazohusiana na mambo ya biashara, matamko ya mabadiliko ya kila wakati kuhusiana na biashara nchini. Nashauri Serikali kupitia upya kauli zake ili kabla haijatoa tamko lolote izingatie mazingira halisi ya wafanyabiashara wetu nchini.