Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa siku ya leo na pia kupata fursa kuchangia. Niipongeze Serikali kwa kazi kubwa na nzuri inayofanya na pia kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na wataalam wote wa Wizara hii, tumeona mabadiliko makubwa ya mtazamo na fikra (mind set change). Nipoongeze na kumshukuru Mheshimiwa Rais kuanzisha Wizara ya Uwekezaji na kazi yao kubwa ni kufanya uratibu baina ya Wizara zote kuhakikisha kunakuwa na mazingira wezeshi na bora katika uwekezaji ambayo ni muhimu kwa suala la biashara na pia viwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nishauri katika maeneo machache; kwanza Serikali iharakishe kutekeleza Blue Print. Jambo hili linahitaji uratibu wa Wizara zote na utafanya gharama za uzalishaji zipungue bila kuathiri ubora na viwango. Nashauri Serikali iunganishe Taasisi za Udhibiti kuwa mbili, muundo wa juu na muundo wa chini. (Upper Stream Regulatory Authority na Lower Stream Regulatory Authority) na taasisi hizo zifanye majukumu yao ya udhibiti na zisiwe taasisi za kuwa chanzo cha mapato.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii taasisi hizi ndizo kikwazo kubwa cha kufanya urahisi wa kufanya biashara (Ease of doing business) na pia (cost of doing business) kupunguza gharama za uzalishaji. Pia tunashauri Maafisa Biashara ngazi ya Taifa, ngazi ya Mkoa, ngazi ya Wilaya ndio wawe sehemu ya kutoa leseni na ushauri wote unaohitajika kufanya biashara yoyote (one stop center). Pia pawe na kanuni ya kubana utoaji wa adhabu (fine) ili kwanza mtu apewe fursa ya kurekebisha kabla ya tozo ya adhabu.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia Serikali iwekeze katika kuelimisha kupitia taasisi zetu za elimu ya ufundi, SIDO, TEMDO na pia katika Taasisi ya Utafiti - TIRDO. Bila utafiti hatutaweza kuwa na mafanikio. Tunaomba SDL, fedha zote asilimia nne na nusu 4.5% ziende katika kuboresha taaluma ya ujuzi kwa vitendo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni muhimu Serikali tuwekeze katika Sekta ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ili kukuza ajira, biashara na kupatikana kwa malighafi ya viwanda vyetu. Muhimu kupata utafiti wa bidhaa tunazoagiza kutoka nje ambazo tunaweza kuzalisha ndani ya nchi ili tuweze kuzalisha ndani ya nchi badala ya kuagiza nje. Leo hii Serikali itaona sekta isiyokuwa rasmi inakua kwa kasi kubwa na sekta rasmi kushuka kwa sababu ya kutokuwa na mazingira na usawa wa kufanya biashara. Napongeza na kushukuru jitihada zote za Wizara na wataalam wote. Siku zote changamoto ndogo ndogo zitakuwepo na ni kuangalia namna ya kuboresha na kuondoa hizo changamoto.