Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kupata nafasi ili niweze kutoa maoni yangu kwenye Wizara hii muhimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na watendaji wote wa Wizara kwa mchango mkubwa wanaoutoa kwenye Wizara hii. Wizara ya Viwanda na Biashara ndiyo yenye jukumu la kusimamia Sera ya Viwanda na Biashara nchini na Wizara nyingine ndiyo watekelezaji. Kwa hali ya kawaida, Wizara ya Kilimo ndiyo tulitegemea ichangie sana au zaidi kwenye maendeleo ya viwanda hapa nchini. So far Wizara ya Viwanda haina direct link na Wizara ya Kilimo.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi kama Taifa tunategemea kuingiza mafuta ya kula kutoka nje. Sasa Wizara ya Viwanda inge-link na Wizara ya Kilimo tungehakikisha tunakuwa na mbegu bora na kuweza kuzalisha mafuta ya kula hapa nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2018 tulizindua mradi wa ASDP II na mradi huu una pesa nyingi sana. Tungekuwa na link na Wizara ya Kilimo ingetusaidia sisi kama nchi kuweka mkakati mzuri wa kuzalisha products zetu badala ya kutegemea bidhaa kutoka nje.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati umefika sasa kuhakikisha tunatengeneza soko la ndani. Lazima taasisi za kiserikali wapewe tamko rasmi kuhakikisha vitu vyote ambavyo vinatumiwa na hizi taasisi za kiserikali watumie bidhaa ambazo zimezalishwa hapa nchini. Tanzania ya Viwanda inawezekana kwani lazima tujipange vizuri na sector zote nchini lazima zishirikiane.

Mheshimiwa Naibu Spika, niwatakie kheri Mheshimiwa Waziri na watendaji wote katika utekelezaji wa bajeti yao. Naunga mkono hoja.