Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Sonia Jumaa Magogo

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. SONIA J. MAGOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kwa kuwapongeza watendaji wote wa Wizara kwa jitihada kubwa wanazozifanya kuendeleza sekta hii ya viwanda na biashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, niiombe sana Wizara iiangalie Tanga kwa jicho la huruma kabisa. Mkoa wetu unazalisha matunda kwa kiwango kikubwa sana tena mengine ambayo huwezi kuyapata mahali pengine popote tatizo hatuna kiwanda. Matunda yanaoza sana na kusababisha hasara kubwa kwa wananchi, hivyo Serikali iwasaidie wananchi hawa kuondokana na tatizo hili na kukuza wigo wa biashara na uchumi kwa Mkoa wa Tanga.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia tunaomba tupatiwe kiwanda kwa ajili ya nafaka kama mahindi, mihogo, ambayo inalimwa kwa kiasi kikubwa sana katika Mkoa wa Tanga. Kuna viwanda vinasuasua sana kama cha chuma, kamba hakiko vizuri kabisa kwa sasa. Pia tungeomba turejeshewe viwanda vya mbolea na plastic ambavyo vilihamishwa hivyo kudororesha kwa kiasi kikubwa uchumi wa Mkoa wa Tanga.