Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Gibson Blasius Meiseyeki

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arumeru-Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. GIBSON B. MEISEYEKI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia Wizara hii. Nianze kwa kusema kwamba mimi ni Mjumbe wa Kamati hiyo ya viwanda na biashara lakini pia mimi ni mjasiriamali.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye vikao vyetu hivyo vya Kamati wakati mwingine tunapatwa na bumbuwazi kwa jinsi ambavyo kero hizi ambazo wafanya biashara na wawekezaji wanazipata katika nchi yetu. Kwa kweli hali ni mbaya ya kibiashara sasa hivi nchini na sisi humu ndani tumezidi kulia. Tumekuwa kama watu wa kulia tu na narudia kusema kwa sababu nimeshasema hivyo kipindi cha nyuma, ifike mahali tuisaidie Serikali na tuisaidie nchi yetu humu ndani.

Mheshimiwa Naibu Spika, wengi wamechangia kwa masikitiko sana humu ndani ya Wizara hii, sasa ufike wakati baadaye wakati tunapitisha hapa tumsaidie Waziri, baadhi ya kero hizi ambazo wafanyabiashara wamekuwa wakilia zitatuliwe humu humu ndani, tusiipitishe hii Bajeti leo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wafanyabiashara wanalalamikia sana, kwa mfano, suala la ETS hizi electronic stamp, ni kazi ya TRA lakini wanaogharamia ni wazalishaji, kwa nini msilipe wenyewe? Kwa sababu hizo stamp ni kwa faida yenu nyie kujua production za viwandani. Wanalalamika kwamba hizi fedha ni nyingi zinasababisha wanashindwa kukuza mitaji yao. Leo Waziri na Serikali humu ndani ifute hiyo ili tuweze kusonga mbele. Wengine wanasema hata matangazo ya biashara zao wanaweka mabango barabarani, TRA wanakusanya kama ni maeneo ya TARURA na wenyewe wanakuja wanakusanya fedha, sasa hawa watu watakuza mitaji yao lini? Kama inawezekana achaji mmoja mwingine abaki, kwa sababu TRA na TARURA ni organ ambazo zinaweza kufanya kazi pamoja kwa nini wanadaidai wafanyabiashara? Hivi viwanda vyetu vya ndani visipotangaza biashara zao watapataje masoko? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Komu hapa, kama siyo yeye ni nafikiri ni Mheshimiwa Japhary alisema ng’ombe ili aweze kupata maziwa lazima umlishe, lakini sisi hapa hatuwasaidii wafanyabiashara, tunawakwamisha na in fact na hali ya nchi yetu sasa hivi Kimataifa siyo nzuri kwa maana ya uwekezaji, is not good. Sasa tunaongea, tunalia halafu tukiondoka, mwakani tena tunaendelea hivyo hivyo. Nashauri kwamba Bunge hili leo liisaidie Serikali, tuwasaidie wananchi wetu, tuna vijana wengi wanamaliza Vyuo Vikuu kama wenzangu walivyotangulia kusema, hatujui wakitoka hapo wanakwenda wapi. Uwekezaji tunau-discourage badala ya kuu-promote.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo naomba kwamba leo tumsaidie, maana najua alikuwepo hapo Mheshimiwa Charles sasa hivi tunaye Kakunda, kuna wakati unaongea anakuangalia tu. Kuna namna hawawezi, wanashindwa, hawana cha kufanya. Kuna wakati umefika hapa tukafikiria pengine na wafanyabiashara wa nchi hii tuwakutanishe na Rais ili baadhi ya kero wazimalize pale pale on the spot maana yake hapa ndani tunaona tunazungusha tu, muda unakwenda, hakuna uwekezaji, tunaendelea kuzalisha vijana, hawapati ajira, sasa naona sisi kama Wabunge tuna nafasi yetu hapa badala ya kulialia tu tunaweza tukahitimisha haya mambo humu humu ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo hapa Waziri wa Fedha atuambie ETS wanaifanya vipi, habari ya mabango na kero nyingine hizo za kodi ambazo zimetamkwa hapa ndani, hizo kodi tu-harmonize akina OSHA na nashukuru Rais alivyokuwa kusini mwa nchi hii alishangaa nay hii OSHA maana yake ni nini. Anatoka OSHA, anaingia sijui mtu wa levy, msururu wa watu, kila siku wapo maofisini kwa watu. Wawekezaji tulionao hapa nchini kama hawatuzungumzii vizuri hatutapata wawekezaji wapya. Ni lazima tuhakikishe hawa tulionao tunawa-contain vizuri ili wanapoulizwa kuhusu uwekezaji Tanzania waweze kutu-advertise, waweze kuitangaza Tanzania kama ni sehemu nzuri ya kuwekeza, lakini sasa hivi tunapata negative comments kwamba Tanzania siyo sehemu nzuri ya kuwekeza. Sasa tutakwenda wapi na watoto ambao tunawazaa?

Mheshimiwa Naibu Spika, bidhaa zetu za ndani; najaribu kupata picha hivi watu wote humu ndani tungekuwa Wamasai tukawa tunavaa yale mashuka ya Kimasai ni viwanda vingapi vingekuwepo sasa hivi Tanzania vingekuwa vinajaribu kutuvalisha hizo nguo? Humu ndani tumevaa masuti tu hizi siyo products za Tanzania. Ifike mahali tuwe na utashi wa kisiasa na tuanzie humu Bungeni. Hebu tuondoeni haya matai tai na masuti ambayo ni ya kuagiza tuvaeni nguo za kwetu... (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)