Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, barabara, maeneo ya uzalishaji. Pamoja na jitihada za kuunganisha mikoa kwa mikoa, nashauri na kupendekeza Serikali iongeze nguvu kwenye maeneo ya uzalishaji kiuchumi ili kuchochea shughuli za uzalishaji na hivyo kuongeza Pato la Taifa. Mfano, Wilaya ya Mufindi, Barabara ya Mafinga kwenda Mgololo ni uti wa mgongo wa uchumi kuelekea kwenye Viwanda vya Chai, Karatasi na Mazao ya Misitu. Wakati wa mvua unakuta malori yamekwama kwa wiki nzima, hii maana yake ni ku-slow down speed ya uzalishaji na hasa usafirishaji.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Mufindi inachangia Pato la Taifa kwa kuwa miongoni mwa wilaya tano bora kimapato. Pamoja na hali hii, bado inaweza kuchangia zaidi ikiwa barabara hii itapitika mwaka mzima. Hivyo, nia yangu hapa ni kuishauri Serikali kuwa itazame maeneo ya kimkakati kiuchumi hata kama maeneo haya hayaunganishi mkoa kwa mkoa.

Mheshimiwa Spika, mawasiliano; Mji wa Mafinga ni mji wa kibiashara na unakuwa kwa kasi sana kutokana na uwepo wa shughuli za viwanda vya mazao ya misitu. Hata hivyo, kuna maeneo ambayo ni just about or less than 15 kilometres from Mafinga Town, hakuna mawasiliano. Mawasiliano ni component muhimu kwenye shughuli za kiuchumi na purchasing power iko juu, wakipata mawasiliano yatachangia uchumi kwa kununua data na muda wa maongezi. Hivyo naomba mawasiliano katika Vijiji vya Kisada, Bumilayinga, Ulole, Kikombo, Maduma na Itimbo.