Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Spika, naomba nichangie katika hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, uwanja wa ndege; kwa kuwa Kiwanja cha Ndege Njombe kiko katika hali mbaya, niombe Serikali ikarabati kiwanja hicho. Serikali imekuwa ikisema iko kwenye mchakato lakini sasa ni miaka minne Wananjombe wanajibiwa kuwa kiko kwenye mchakato.

Mheshimiwa Spika, Barabara za Itoni – Ludewa (Njombe) – Njombe – Makete. Hali ya barabara zile sio nzuri, hasa kipindi hiki wakati wa mvua. Naomba wakandarasi walipwe kwa wakati ili waweze kuharakisha ujenzi wa barabara hizo.

Mheshimiwa Spika, mawasiliano ya simu; maeneo mengi ya Jimbo la Lupembe hakuna mawasiliano ya simu mfano Madeke, Kanikerere na maeneo mengine. Naomba Serikali iwasaidie wananchi kupata mawasiliano.

Mheshimiwa Spika, miradi kushirikisha Sekta Binafsi; kwa kuwa miradi mingi inasuasua kwa sababu Serikali peke yake inagharamia. Ili kuharakisha maendeleo, nashauri miradi hiyo washirikishwe sekta binafsi kwani sekta hiyo wakipewa miradi hiyo wataharakisha kumaliza miradi hiyo.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.