Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Amb Dr. Diodorus Buberwa Kamala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. BALOZI. DKT. DIODORUS B. KAMALA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Katika Jimbo la Nkenge, Wilaya ya Misenyi tuna ahadi tano muhimu za viongozi wetu ambazo zilitolewa wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu uliopita. Naomba nimkumbushe Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano achukue hatua za haraka kutekeleza ahadi hizo. Ahadi hizo ni pamoja na:-

Mheshimiwa Spika, kwanza, kuongeza kasi ya ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Katoma hadi Bukwali. Barabara hii ni muhimu sana na inaunganisha Tanzania na Uganda. Ni ahadi ya Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Spika, pili, kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Kajai hadi Hospitali Teule ya Wilaya ya Mugane. Ni ahadi ya Mheshimiwa Makamu wa Rais.

Mheshimiwa Spika, tatu, barabara ya Mutukula hadi Minziro, kujengwa kwa kiwango cha lami. Ahadi hii ilitolewa na Mheshimiwa Rais alipozindua one boarder post ya Mutukula.

Mheshimiwa Spika, nne, barabara ya kutoka Kituo cha Afya cha Kabyaile hadi Gera. Ahadi hii ilitolewa na Mheshimiwa Rais alipotembelea Kituo cha Afya cha Kabyaile.

Mheshimiwa Spika, tano, ujenzi wa kiwango cha lami wa kilometa tatu za lami Makao Makuu ya Wilaya (Kyaka – Bunazi). Ahadi ya Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.