Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ZAINABU M. AMIRI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote nampongeza Mheshimiwa Isack Kamwelwe, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Pamoja na Naibu Waziri Mheshimiwa Atashasta Nditiye kwa juhudi kubwa wanazozifanya katika kusimamia miradi mbalimbali katika Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali iweke vifaa vya uokoaji maeneo ya barabara kuu, mfano, gari la zimamoto, winchi, magari ya breakdown ili kuweza kusaidia uokoaji pindi ajali itokeapo na pia kuondoa msongamano barabarani wa magari endapo gari litapinduka na kuzuia magari, itachukua muda mfupi kushughulikia zoezi la kutoa gari hilo na magari kuendelea na safari.

Mheshimiwa Spika, pia naishauri Serikali ifanye ukaguzi wa mara kwa mara hususan SUMATRA katika magari ya mizigo (maroli) ili kuona ubora wake maana mengi ni machakavu pia ubebaji mzigo mara nyingi ni hatarishi kwa vyombo vingine vya usafiri. Mara nyingi magari haya hutazamwa uzito wa mzigo uliobeba katika mizani tu, ukilinganisha na magari ya abiria ambapo kila kituo kikubwa cha mabasi, hufanyiwa ukaguzi.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali itoe elimu ya kutosha hasa katika magari makubwa ya mizigo kwa madereva wake, kuacha tabia ya kupaki maroli pembezoni mwa barabara mahala pasipostahiki, mfano Kibaigwa, Chalinze na kadhalika (double parking) na kupelekea usumbufu kwa magari yanayopita maana barabara inakuwa finyu na mara nyingine hupelekea ajali kutokea.

Mheshimiwa Spika, vile vile naishauri Serikali iweke vidhibiti mwendo katika magari ya mizigo maana yanaenda kwa mwendo wa kasi wa kupelekea kusababisha ajari kwa magari mengine, mfano mabasi ya abiria ambayo wamewekwa vidhibiti mwendo na hatimaye kupelekea vifo kwa wananchi wasio na hatia.

Mheshimiwa Spika, naishauri pia Serikali iboreshe viwanja vyote vya ndege nchini ili viweze kufanya kazi kwa masaa 24, yaani usiku na mchana. Viwanja vingi vya ndege mfano, Kiwanja cha Ndege Dodoma wakati wa usiku ndege haiwezi kutua kutokana na ukosefu wa taa za kuongozea ndege.

Mheshimiwa Spika, naishauri vile vile Serikali iboreshe mizani iliyopo maeneo ya Mikese, Morogoro, maana kumekuwa na msongamano mkubwa wa magari na ukizingatia eneo la mizani lipo karibu kabisa na barabara kuu na hii ndiyo sababu, kumekuwa na msongamano hivyo nashauri Serikali iboreshe.

Mheshimiwa Spika, mwisho, nawaombea Mheshimiwa Waziri na Naibu wake afya njema na maisha marefu ili wazidi kutekeleza majukumu yao ya kila siku.