Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ENG. RAMO M. MAKANI: Mheshimiwa Spika, pongezi kwa Serikali kwa upana wake na Wizara kwa namna ya pekee kwa kazi kubwa na ya mfano wanayoifanya, hongera sana.

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Tunduru Kaskazini na bajeti ya mwaka 2019/2020; nashukuru kwa miradi ifuatayo ambayo imetengewa fedha. Ukurasa wa 348, daraja F/ Mbanga – shilingi milioni 20 (ukamilishaji). Nina mashaka na utoshelevu wa fedha hizi kukamilisha kazi iliyobaki kwani bado kazi ni kubwa.

Mheshimiwa Spika, ukurasa wa 348 - matengenezo ya barabara Mjimwema – Ngapa - Tunduru/Nachingwea Boarder – shilingi milioni 60. Barabara hii ni muhimu saba kuunganisha Mkoa wa Ruvuma na Mkoa wa Lindi. Tunaomba ijengwe kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, ukurasa wa 348 - ujenzi wa Daraja la Ngapa katika barabara ya Mindu – Ngapa - Nachingwea/ Tunduru Boarder – shilingi milioni 60. Jumla ya fedha zote ni shilingi milioni 140. Kwa kulinganisha na mahitaji katika Jimbo langu, pamoja na kushukuru kwa tulichopata tunaomba yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, mahitaji ya miradi muhimu sana. Barabara ya Mkoa – Mjimwema - Nachingwea Boarder. Tunaomba ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami, likiwemo Daraja la mto Lumesule.

Mheshimiwa Spika, barabara ya mchepuo (Tunduru- By-Pass), ni bahati mbaya haikupata umuhimu katika bajeti, tunaomba izingatiwe.

Mheshimiwa Spika, Tunduru Round about; hapa kuna barabara inayokwenda Songea, Mtwara na Msumbiji. Makutano ya barabara katika eneo hili, wakati wa ujenzi wa barabara za Tunduru – Matenanga – Namtumbo – NA – Tunduru – Nakapanya – Mangaka - Taaluma na umuhimu, ikiwemo usalama. Tunaomba yafanyike marekebisho ya kitaalam.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Mironde – Kalulu - Selous Game Reserve, ni barabara ya kimkakati; katika ziara yake Waziri Mkuu akiwa Kalulu alielezea umuhimu wake na kusisitiza kwamba Serikali itaijenga.

Mheshimia Spika, nashukuru sana.