Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Mawaziri, Katibu Mkuu na wafanyakazi wote wa Wizara kwa kazi kubwa na ngumu wanayoifanya. Hongereni sana.

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya wananchi wa Urambo, tunashukuru sana barabara iliyokamilika katikati ya Mji wa Urambo. Ahsanteni sana kwa kuongeza uzuri wa mji. Barabara hii nzuri ni muhimu sana ikaunganishwa vizuri pale inapoungana/kuchepuka kutoka barabara inayoendelea Kigoma.

Mheshimiwa Spika, tunaomba round about kwanza kwa usalama wa magari na waenda kwa miguu na pili kwa mwonekano mzuri wa barabara inayoingia mjini.

Mheshimiwa Spika, tunaomba minara ya simu katika maeneo ambayo hayana mtandao wa simu; na orodha ya kata na vijiji imeletwa Wizarani.

Mheshimiwa Spika, tunaomba maombi mawili ya round about na minara yafikiriwe kwa manufaa ya wananchi na Taifa kwa ujumla. Ahsante sana.