Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Emmanuel Papian John

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. EMMANUEL P. JOHN: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja ya bajeti ya Wizara hii ya Ujenzi na Mawasiliano. Nampongeza Mheshimiwa Waziri na Timu yake kwa hotuba na ripoti nzuri.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Kongwa (Hogoro) – Kibaya – Orkesimet – Oljoro – Arusha, ina mpango gani? Tunaomba tujengewe kwa awamu, Kongwa – Kibaya. Sababu ya barabara hii ni kusafirisha mazao toka Chemba, Kiteto, Kilindi na Handeni kwenda Dodoma na Dar es Salaam. Kwa kurahisisha barabara ya Babati – Kibaya – Dar es Salaam, Kondoa – Kibaya – Dar es Salaam, Kilindi – Kibaya – Dar es Salaam, Kilindi – Kibaya – Dodoma, Chemba – Kibaya – Dodoma.

Mheshimiwa Spika, mizigo mingi toka Dar es Salaam kwenda Babati, Simanjiro, Chemba, Kiteto, Kilindi, Kondoa yote inapita hapa. Tusaidieni kwa sababu hii ni too economical.

Mheshimiwa Spika, pia tunaomba kujua barabara ya Handeni – Kiberashi – Kibaya – Chemba – Kondoa – Singida itajengwa lini kwa kiwango cha lami? Umuhimu wa barabara hii ni bomba la mafuta, bandari ya Tanga kwenda Kanda ya Ziwa, kuunganisha Mikoa ya Tanga, Manyara Dodoma na Singida.

Mheshimiwa Spika, naomba Mawasiliano, tupatiwe minara katika Kijiji cha Raiseli, Songambele, Kijunge, Rengatei, Sunya, Dongo, Mangungu na Namelok. Shahidi ni Mheshimiwa Dkt. Kalemani.