Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. Aidha, nawapongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Mawaziri na timu yote ya Wizara katika utekelezaji wa majukumu yao kwa ufanisi pamoja na changamoto za ufinyu wa fedha (bajeti).

Mheshimiwa Spika, katika mradi na ujenzi na reli ya SGR ni muhimu katika vituo vikubwa kama vile Morogoro, Dar es Salaam na Dodoma kungejengwa maeneo makubwa ya kuegesha magari (car parking) ili kuwezesha abiria wanaotoka Dodoma kwenda Dar es Salaam kwa usafiri binafsi, wanapofika Morogoro wanaweza kuegesha magari yao kwenye maengesho hayo, kisha kupanda SGR kwa safari ya Dar es Salaam na hivyo hivyo wanaporudi.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Kidatu – Ifakara – Lupiro – Malinyi – Londo – Lumecha – Songea inapitia katika maeneo muhimu kwa uchumi wa nchi pamoja na mradi SAGCOT (kilimo cha biashara) lakini barabara hii bado haijapewa kipaumbele.

Mheshimiwa Spika, barabara kipande ya Kidatu – Ifakara, ujenzi wa kiwango cha lami unasuasua sana. Sababu ni uzembe wa Mkandarasi. Tunaiomba Serikali itafakari kama kweli Mkandarasi anao uwezo wa kumaliza kazi katika muda muafaka. Aidha, Serikali ilete taarifa ni mkakati gani utafanya katika kumsukuma Mkandarasi kumaliza kazi ndani ya muda.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Ifakara – Lupiro – Malinyi – Londo –Lumecha – Songea imefunguka toka mwaka 2017, lakini haipitiki kabisa kipande cha Mpepo - Londo kutokana na milima haijachongwa. Tunaiomba Serikali irekebishe maeneo korofi yote ili barabara hii itumike kwa kuwaunganisha wakazi wa Mikoa ya Morogoro na Ruvuma.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Ifaka – Lupiro – Malinyi – Londo imetolewa ahadi na Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli katika kampeni zake za uchaguzi mwaka 2015, lakini pia alirudia ahadi hiyo katika ziara yake mkoani Morogoro Mei, 2018 kuanza kujenga kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, Serikali katika majumuisho, naomba itoe maelezo katika kutekeleza ahadi hiyo ya Mheshimiwa Rais kwa wakazi wa Morogoro/Ruvuma. Ahsante.