Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Eng. Christopher Kajoro Chizza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ENG. CHRISTOPHER K. CHIZA: Mheshimiwa Spika, naipongeza Wizara kwa kuleta bajeti yenye vipaumbele vya miundombinu inayochochea ukuaji wa uchumi.

Mheshimiwa Spika, kwenye utekelezaji, kipande cha barabara ya Kidahwe – Kibondo - Nyakanazi kinachotekelezwa kutoka Nyakanazi ni Nyakanazi - Kabingo kilometa 50, siyo Nyakanazi - Kibondo. Nashauri Wizara isahihishe kwa sababu kati ya Kabingo na Kibondo kuna kilometa 50 ambazo hazina Mkandarasi, ndiyo maana kwenye mradi utakaofadhiliwa na AFDB zinaonekana kilometa 260 za Kabingo – Kibondo – Kasulu – Manyovu. (I stand to be corrected)

Mheshimiwa Spika, wakazi wa Mkoa wa Kigoma katika wilaya zote za Kigoma, Uvinza, Kasulu, Buhigwe, Kibondo na Kakonko wanafanyia biashara zao nyingi katika Kanda ya Ziwa, hususan Mwanza na Shinyanga. Naishukuru Wizara kwa kuliona hili na kutenga fedha za kujenga barabara yote ya Nyakanazi – Kabingo – Kibondo – Kasulu - Manyovu ili kuunganisha Mkoa wa Kigoma na mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu ni kama ufuatao:-

(i) Mkandarasi wa Nyakanazi - Kabingo asimamiwe kwa ukaribu, he is very slow. Tulipokagua utekelezaji na Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mkandarasi alikuwa ametekeleza asilimia 60 tu na tayari alikuwa na siku 986 nje ya mkataba.

Mheshimiwa Spika, nashauri kwa kipande cha Kabingo - Manyovu AFDB utaratibu wa fidia uanze mapema.

Mheshimiwa Spika, naomba Wizara itekeleze ahadi ya Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli ya 2015 ya kujenga kilometa tatu za barabara za lami Mjini Kakonko. Kwa maelekezo ya Mheshimiwa Waziri, RC wa Kigoma, kupitia TANROADS ameshatuma Wizara ya Ujenzi makisio ya gharama ya kujenga kilometa tatu za Mjini Kakonko. Chonde chonde, hii ni ahadi ya Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.