Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Katani Ahmadi Katani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tandahimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. KATANI A. KATANI: Mheshimiwa Spika, nichukue fursa hii kuishukuru Serikali kwa kutuongezea kilomita 50 za barabara ya lami kutoka Mnivati – Tandahimba. Ombi langu kwa Serikali ni kwamba kwa kuwa barabara hii ni muhimu kwa uchumi wa Mkoa wa Mtwara ambao unategemea sana zao la korosho huku asilimia 47% ya korosho zote Tanzania zikiwa zinatoka maeneo hayo, Serikali iwape wakandarasi zaidi ya mmoja ili tupate matokeo ya haraka sana.

Mheshimiwa Spika, ikumbukwe tu kuwa tunazo kilomita 50 za awali za kutokea Mtwara kuelekea Mnivati lakini barabara hii ambayo mkataba wake ilikuwa uwe umekamilika ndani ya miezi kumi na saba mpaka sasa ni kilomita 8 tu ndiyo zimewekwa lami. Hii ndiyo kusema kwa kusuasua huku tutahitaji miaka 10 kukamilisha barabara hiyo.

Mheshimiwa Spika, naomba maeneo yafuatayo yapate minara ya simu; Kata za Mdimiba, Michenjele, Nganja, Mkwiti, Mkoreha na Chaume. Kata hizi hazina mawasiliano ya simu, naomba suala hili lishughulikiwe.

Mheshimiwa Spika, niombe kuzungumzia suala la reli ya kutoka Mtwara – Mbambabay - Mchuchuma - Liganga. Reli hii kama itejengwa italeta fursa za kibiashara Kusini mwa Tanzania na nchi za Malawi, Zambia na Msumbiji.