Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Prof. Norman Adamson Sigalla King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. PROF. NORMAN A. S. KING: Mheshimiwa Spika, naomba sana ahadi ya barabara ya kutoka Njombe – Makete - Mbeya ifanyike. Kutoka Makete ni barabara ya kutoka Makete - Bulongwa – Mbeya na Makete- Ivalalila - Ujuni kuunganisha barabara ya kutoka Bulongwa.

Mheshimiwa Spika, pia kwa ajili ya kuwezesha Hifadhi ya Kitulo ni muhimu barabara ya kutoka Chimale- Matemba au Mfumbi kuja Matamba ijengwe kwa lami. Pia ili kuboresha ujenzi wa barabara za Ludewa, Kipengele- Mbalache - Lupila kwenda Ludewa ijengwe kwa lami.

Mheshimiwa Spika, kuhusu mawasiliano Kata za Mang’ota, Ikuwo, Kigala, Lupila na Ukwama zipewe mawasiliano ya Voda, Airtel, Halotel na Tigo. Hili likifanyika litasaidia sana kutupa mawasiliano.