Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. OMARI A. KIGODA: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa niipongeze Wizara na Mawaziri wake kwa kazi bora.

Mheshimiwa Spika, kipande kilichobaki cha Mziha - Handeni kwenye majibu ya Waziri kilitengewa shilingi bilioni 2, katika kitabu cha hotuba ya Waziri ukurasa wa 29-30 ameeleza Serikali bado inatafuta hela. Naomba kwenye majumuisho nipate ufafanuzi wa suala hili hasa akizingatia wananchi wa Handeni na Tanga kwa ujumla wamepata faraja baada ya kusikia imeshatengwa shilingi bilioni 2 kutokana na majibu ya Wizara.

Mheshimiwa Spika, barabara nyingine yenye umuhimu mkubwa ni ile ya Handeni – Kiberashi. Hii barabara ndiyo litakapopita bomba la mafuta. Naomba ufafanuzi wa Serikali kuhusu barabara hii kujengwa kwa kiwango cha lami hata tukianza kwa vipande vipande itasaidia.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.