Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Spika, Mji wa Geita ulipewa ahadi na Mheshimiwa Rais kujengewa kilomita 10 za lami. Mwaka jana nilipoongea na Waziri aliahidi kuziweka kwenye bajeti ya mwaka huu wa 2019/2020. Nimeangalia kwenye kitabu lakini hakuna barabara zangu. Namwomba sana Mheshimiwa Waziri anionee huruma hii ni ahadi ya Rais ambayo kwa miaka yote minne imekuwa inaonyeshwa kwenye vitabu lakini barabara hazijengwi. Kwa heshima kubwa, naomba jambo hili Waziri alipe umuhimu wake.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.