Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ENG. GERSON H. LWENGE: Mheshimiwa Spika, awali ya yote, naunga mkono hoja ya Waziri na nampongeza sana Waziri, Naibu Mawaziri na vviongozi wote wa Wizara hii kwa hotuba yenye kuleta mabadiliko makubwa katika kujenga miundombinu itakayotufikisha kwenye uchumi wa kati.

Mheshimiwa Spika, pamoja na pongezi hizi, naomba Waziri arejee kwenye barabara ya Njombe (Ramadhani) – Igwachanya – Iyayi ambayo ni barabara muhimu kwani inaunganisha Makao Makuu ya Mkoa na Makao Makuu ya Wilaya ya Waging’ombe (Igwachanya). Pia inapita maeneo muhimu ya utalii ya msitu wa asili wa Nyumbanintu na Hifadhi ya Pori la Akiba la Mpanga/Kipangele pale Ludunga na kuunganisha na TANZAM Highway pale Igando. Barabara hii ilishafanyiwa upembuzi na usanifu wa kina toka mwaka 2014 ilipokamilika na ipo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2015.

Mheshimiwa Spika, naomba pia Wizara ione uwezekano wa kuongeza kiwango cha lami pale Igwachanya ambapo ni Makao Makuu ya Wilaya. Nimeona imepangwa kujengwa mita 100 tu kwa bajeti hii 2019/20. Kumleta mkandarasi kuja kujenga mita 100 itagharimu pesa kubwa kwani kuleta mitambo ya kujenga mita 100 haina tofauti na ile ya kujenga kilomita 5. Naomba tupate angalau kilomita 2.

Mheshimiwa Spika, sijaona mpango mahsusi na kuboresha Uwanja wa Ndege wa Njombe. Mkoa wa Njombe unahitaji kupata uwanja mkubwa wa ndege. Huu ulipo ni mdogo na pengine itakuwa vigumu kuupanua kwa kiwango kikubwa.

Mheshimiwa Spika, nashauri toka bajeti ya 2018/2019 kuwa Wizara ijaribu kwenda pale Ilembula Hospitali tunao uwanja wa ndege na ardhi ya kutosha ambapo ingeweza kujenga uwanja mkubwa wa ndege kwa kiwango cha uwanja wa ndege wa mkoa. Hakutakuwa na gharama kubwa ya fidia kama kupanua ule Uwanja wa Njombe Mjini ambapo majengo mengi ya kudumu yamejengwa.