Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa dakika hizo tano, lakini mimi pia ninaona tu kwamba ninamshukuru Mungu kwa sababu ili la Bagamoyo miongoni mwa nondo ambazo pia ambazo nilikuwa nimeziandaa nilikuwa nimejiandaa sana kuja kuchangia katika hii project ya Bagamoyo kwanza nikushukuru wewe binafsi kwa uzalendo mkubwa ambao umeuonyesha kulizungumzia hilo, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, mimi nakumbuka mwaka 2012 alipokuja Rais wa China kabla ya hapo Serikali hii ya Chama cha chetu cha Mapinduzi mwaka 2008 ili hire consultant ambaye alifanya kazi ya kufanya feasibility study wakaja na recommendation za ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo, lakini kama alivyosema mama yangu Nagu kipindi hicho mimi nilikuwa chini ya Wizara ya Viwanda nilikuwa nikifanya fair competition, Mama Nagu alikuwa bosi wangu, nataka nikuambie kitu kimoja not only kwamba hii Bandari ya Bagamoyo tunaizungumza hapa kwamba ilikuwa ina muhimu, lakini ilikuwa inakwenda kuwa the biggest port in Africa.

Mheshimiwa Spika, namba mbili Bandari hii ya Bagamoyo ilikuwa inakwenda kufanya circulation ya kuingiza makontena zaidi ya milioni 22 kwa mwaka ukilinganisha na Bandari ya Dar es Salaam, kwa wachumi waliokuwa wamefanya feasibility study pamoja na consultant, bandari hii ilikuwa inakwenda kuwa hub ya kuzifungua nchi ambazo ni land locked na mradi huu, nataka nikwambie ulikuwa unakwenda kuongezwa, wawekezaji hawa walikuwa wanakwenda kujenga Standard Railway Gauge ambayo ilikuwa inakwenda ku-connect kutoka Bagamoyo mpaka kwenye Reli ya TAZARA.

Mheshimiwa Spika, mimi nataka nikwambie ndugu zangu wa Serikali mimi ninawaomba hapa sisi kama Wabunge ni wawakilishi wa wananchi kwa maslahi ya hili Taifa, hatuwezi tukaja hapa Bungeni tukazungumza kwa lengo la kuikwamisha Serikali, nimesoma kitabu hichi, kinachozungumzwa ni kwamba inaonekana kwamba mkandarasi sijui kuna mambo hayako kwa maslahi ya nchi, hatuwezi tukaishia hapo tu, tuangalie vipengele ambavyo vinakwamisha tuviondoe, mradi huu ukatekelezwe kwa maslahi ya hili Taifa.

Mheshimiwa Spika, leo Rais tayari Serikali yetu imeanza kujenga Standard Gauge Railway kutoka Morogoro - Dar es Salam kuja Dodoma, kama tutafanikisha mradi huu tayari hii Reli ya Standard Gauge itaweza kupata access ya kuwa fade na mizigo ambayo tutaichukuwa kutoka Bandari ya Bagamoyo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo mimi kwa unyenyekevu mkubwa ninaungana na Wabunge wengine kuisisitiza Serikali this is the grand project kama Spika ulivyosema, tunaishauri Serikali ikakae iangalie wapi tumekwama mradi huu uweze kutekelezwa.

Mheshimiwa Spika, la pili naomba niende jimboni. Katika jimbo langu la Singida Magharibi na Mheshimiwa Waziri nimeshakuona zaidi ya mara tatu mwaka jana watu wangu wa Kata ya Iyumbu walivamiwa na majambazi saa tisa mchana, maduka yakaporwa kila kitu, watu wakakosa access ya kufanya mawasiliano hata polisi kuja kuwasaidia, hakuna minara ya mawasiliano. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwaka jana tumeletewa kitabu hapa na hili lazima tuliseme, Serikali Watanzania pia wanaona, msiwe manakuja hapa jamani wakati mwingine mnatupiga longolongo tunapata shida huko, tuliletewa vitabu hapa vinavyoonesha takwimu za minara itakayokwenda kujengwa na makampuni ikiwemo TTCL, mpaka leo tunapozungumza, wale wananchi wangu mimi kutoka makao makuu ya Wilaya mpaka ufike Kiyumbu ni zaidi ya kilometa 190 hawana minara ya mawasiliano, makampuni ya private mmeyazuia, sasa tunataka TTCL ikuwe lakini it must be competitive ili tuweze kuwasaidia watu wetu.

Mheshimiwa Spika, la pili kwenye kitabu nimeangalia barabara inayojengwa kutoka Sepuka - Mlandala kwenda Mgugila, ninaomba nimalizie hili kwa uchache sana, barabara hii nimeanza kuiona toka nikiwa Mkuu wa Wilaya ya Igunga mwaka 2012/2013; imejengwa madaraja yasiyopungua 40, ni mwaka wa kumi hii barabara Serikali wameshindwa kuipandisha/kuijengea tuta la moramu, leo naangalia kwenye kitabu imeombewa milioni 90.

Mheshimiwa Spika, mimi naiomba Serikali wananchi hawa wa Iyumbu, Mheshimiwa Waziri nimeshakufuata zaidi ya mara mbili.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Ikungi asilimia 90 ya revenue inapata revenue kutokana na wakulima wanaotoka kwenye Jimbo langu Singida Magharibi kwa sababu tunazalisha mpunga na mchele kwa kiwango kikubwa, lakini wananchi hawa tumeshindwa kuwakamilishia ujenzi wa hii barabara for ten years madaraja yamejengwa. Mimi nasema safari hii sitaingua mkono bajeti ya Wizara hii kama sita pata majibu ya ujenzi wa barabara ya watu wangu kwa sababu watu hawa wamekuwa wakipata shida, nimekwenda personal kulizungumza nimefanya njuhudi na sijapata majibu yoyote nashukuru sana.