Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. DKT. CHARLES J. TIZEBA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru sana kwa kunipa nafasi nami ya kuchangia hoja iliyopo mbele yetu. Kwa sababu ya muda, mengine niliyopanga kusema nitaya-skip na nijikite katika mambo matatu hivi ambayo naamini kwamba yana umuhimu mkubwa Serikali kuyapima na kuona kama inaweza kuyafanyia kazi kwa haraka.

Mheshimiwa Spika, moja, ume-pre-empty mazungumzo niliyotaka kufanya ya Bandari ya Bagamoyo, lakini kwa vile na wewe uliamua kuchangia siyo mbaya. Bandari hii ndiyo itakayokuwa pekee ya kupokea mzigo utakaosafirishwa na SGR, Dar es Salaam haina huo uwezo. Amesema vizuri sana Mheshimiwa Ally Saleh kule, Bandari ya Dar es Salaam tutake, tusitake, hata tuki-dredge namna gani pale Magogoni, turning base inayoweza kupatikana haiwezi ku-accommodate post panamas na forth na fifth generation ya meli zinazotengenezwa sasa, lakini Bagamoyo ndiyo ilikuwa jibu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, haya mambo yaangaliwe upya tu, yaani tusifike mahali tukalikatia tamaa hili jambo. Naishauri Serikali yangu na naipenda, wafanye kuangalia upya suala la Bagamoyo haraka iwezekanavyo kwa sababu tutakamilisha ile SGR, hatutakuwa na mahali pa kushushia mzigo, tutaonekana kituko. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la pili ni Mfuko wa Barabara; Mfuko wa Barabara wameusema wengi katika kuchangia hotuba ya TAMISEMI, lakini mahali penyewe ni hapa kwa sababu Act ya Mfuko wa Barabara ipo chini ya Wizara hii ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano na ule mgawanyo wa 70 kwa 30 umepitwa na wakati. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitasema neno moja tu, mtu akiwa na matatizo ya mishipa ya damu, mishipa mikubwa huwa hai-clot/haipati obstructions, inayopata obstructions ni mishipa midogo midogo (arteries) na hiyo ndiyo husababisha kifo. Sasa sisi tuki-concentrate sana na barabara kuu tukasahau kwamba barabara kuu hazina maana kama barabara ndogo hazifikishi watu na mizigo kwenye barabara kuu na lenyewe hili tunakosea. Iangaliwe upya tu, waangalie kwamba kama sasa ni 50 au 60, 40 lakini kuna kila haja ya kuongeza fedha kwa upande wa TARURA; sasa hivi ilivyo TARURA haiwezi ku-function. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la tatu, nataka kuzungumzia watoa huduma wanaitwa DSTV. DSTV hawa wanatoa huduma kama ving’amuzi vingine, wanatoa huduma kama kampuni za simu, kama umeme na kadhalika. Software ya kumfanya mtu aliyelipia atumie kadiri anavyolipia zipo lakini ndugu zetu hawa wao wana-charge kwa mwezi, ukishalipia ile subscription hata ukafunga king’amuzi, baada ya mwezi ukienda kimekwisha unatakiwa ulipe tena. Sasa mimi sitaki kuuita wizi kwa sababu tunalipa kwa halali, lakini huo ni wizi. Hizi simu tuna-recharge vocha, mbona wao hawatuambii uki-recharge baada ya siku 5 imekwisha automatically, wao kitu gani kinashindikana kwamba nikiwa nimezima king’amuzi maana yake mita haisomi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa nimemaliza hayo, naomba nizungumzie jimbo langu kidogo. Ukurasa wa 300 katika kitabu cha hotuba ya Waziri, imetajwa barabara ya Sengerema- Nyehunge-Kahunda. Hii barabara natarajia inapaswa kufanyiwa upgrading na siyo feasibility study na detailed design, namwomba Mheshimiwa Waziri aangalie hayo maneno yaliyo kwenye mabano yanatofautiana na uhalisia uliopo kwa sababu hiyo hatua ya feasibility study na detailed design imekwishapita na huku ameweka katika miradi kwa hiyo, hawawezi kurudia mradi huo ambao tayari umekwishakamilika. Naamini ni typo tu, kinachotakiwa hapa kuwepo na naomba hili katika kuhitimisha anifafanulie yaani anihakikishie kwamba ni upgrading na siyo habari ya feasibility study na detail design. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwisho; naomba kuzungumzia vivuko; nimesoma kitabu vipo vivuko vinajengwa, lakini kuna kivuko cha Kome – Nyakalilo, zimeenda tume mbalimbali pale. Sitaki na mimi kubashiri vifo, ndugu yangu Mheshimiwa Mkundi alibashiri ajali kule Ukara na ikatokea, sasa mimi hayo maneno sitaki kuyasema, itoshe tu kusema kwamba hicho kivuko hakitoshi watu ni wengi. Kome leo ina watu karibia 120,000 wanavushwa na kivuko cha tani 35, ukiuliza kwa nini kivuko kingine hakijengwi? Fedha hakuna, fedha tunayozungumzia ni shilingi bilioni mbili au tatu, watu pale wakiteketea sijui nani ataulizwa.

Mheshimiwa Spika, nilimweleza Mheshimiwa Kamwelwe tulipokuwa Ukara kwamba hicho kivuko hakifai, Mheshimiwa Kwandikwa amefika mwenyewe; tume iliyoundwa na Serikali baada ya MV Nyerere kuzama imefika pale Nyakalilo, nimeshangaa kweli kwamba humu ndani hakuna mazungumzo ya eneo hilo, halafu nikisimama kupinga bajeti nionekane mkorofi? (Makofi)