Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kweli sehemu yangu kubwa ya mchango wangu utakuwa ni kuhusu bandari ya Bagamoyo ambayo umeitaja hapo. Lakini kwanza nitapitia in passing tu. Kuhusiana na ATCL nakubaliana 100 kwa 100 na mchango wa Mheshimiwa Kapteni Abbas Mwinyi wa wiki iliyopita ametusemea wengi na amesema mengi na amesisitiza yale ambayo opposition tumekuwa tukisema lakini Serikali ilikuwa haitusikilizi naamini kwa kuwa yametoka kwao sasa labda pengine utasikiliza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili ni kuhusiana na reli nakubaliana na wengi ambao wanaosema kwamba reli ni muhimu lakini haiondoshi kuwepo na taratibu nyingine za usafiri. Marekani mizigo mingi inasafirishwa kwa magari makubwa hata kuliko reli, reli ni ya pili, pia kutegemea reli kwa abiria ni makosa makubwa sana, reli ni mizigo, yupo mtu alisema hapa kuna haja ya kuwa na drive ports kila baada ya eneo ili kurahisisha mizigo kuwa collected ili kwenda sehemu nyingine ya nchi au nchi jirani. Kwa mfano kuwa na drive port Dodoma au kuwa na drive port Morogoro ili mizigo inatuliwa pale kisha reli inabeba. India mizigo ni 80 percent ya reli inatia faida kwa 80 percent. Abiria ni less labda 15 percent, mizigo mingine midogo ndio percent iliyobakia, kwa hiyo tusijidanganye reli ni mizigo bila mizigo hakuna reli itakuwa hasara tupu.

Mheshimiwa Spika, la tatu nataka kuzungumzia juu ya suala la mabaharia, nchi yetu mwaka jana tuliridhia mikataba miwili Maritime Law Conventional na Seafarers ID. Lakini hatukwenda mbali zaidi kuleta sheria kuibaidilisha ile sheria ya meli ili iweze kufaidika. Kwa hivyo kwa maana nyingine tumeridhia conventional lakini hali ya mabaharia wetu 5,276, iko mbovu vilevile bila kitambulisho, bila sheria ya kupitishwa hapa haiwezekani mabaharia wetu wakafaidi malipo mazuri ambayo wanaweza kulipwa na wanaendelea kupunjwa kwa sababu tu kwamba sheria haikufuatiliwa domestication I mean mkataba wa Kimataifa hawakufuatilia domestication ya sheria ili mabaharia wetu wawe na hadhi kamili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya hayo nakwenda kwenye Special economic zone ya Bagamoyo, na naanza kwa kusema kwamba tunafanya makosa kama Bunge na kama nchi kuachia miradi mikubwa kama hii ikafutwa bila kuwepo na public discussion. Vilevile nataka nikushawishi hata wewe kwa nafasi yako unaweza kuunda vyombo au kuunda namna ambayo ya kuweza kuchunguza kwa nini kama nchi tunaacha mradi huu ambao tutauelezea leo hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mradi huu kwanza tunaondokane na dhana kwamba ni bandari, ni zaidi ya bandari ni mji, ni ajira ni kufunguka kwa uchumi wa Tanzania. Kutakuwa au kungekuwa na viwanda 800 ambavyo tayari viko pale pale katika eneo kwa hivyo mzigo unachukuliwa unatiwa katika meli unapelekwa nje au mwingine unatoka pale unakwenda Silama unaunganishwa na reli hii mpya ya SGR inakwenda kwingine inakwenda kuuzwa. Pia utajenga Mji wa Kisasa Bagamoyo kwa maana mbili, kwa maana ya kupata watu kuishi lakini pia Dar es Salaam itapumua, Dar es Salaam ikipumua watu wanakwenda kule kuishi Bagamoyo kwa hivyo nchi inatononoka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la tatu kutakuwa na logistic la tan trade ambayo itafanyika itakuwa kubwa sana bandari ya Bagamoyo kama ingejengwa au kama itajengwa itaweza kuchukua makontena milioni 420 kwa mwaka. Sasa hivi bandari kubwa duniani Rotterdam inachukua milioni 11.87, kwa maana nyingine bandari ya Bagamoyo ingebakia kuwa kubwa pengine kwa miaka 100 ijayo kwa Dunia nzima. Rotterdam wanaingiza meli 3,613,315 kwa mwaka kwa maana ya meli 110, hapa ndipo unaweza kuona suala la locally country linaweza kuwa pana. Imagine meli 100 zinakuja kwa siku wanataka maji, wanataka matunda, wanataka toilet paper, sijui wanataka kitu gani imagine faida ambayo ingepatikana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia Bandari hii au eneo hili lingeweza kuzalisha ajira zaidi ya 120,000. Eneo la Dar es Salaam kusema una forfeit kule ambako mkopo unatoka China na Oman marafiki zetu wakubwa tuseme pia suala la demokrasia katika hili wanatuunga mkono katika mambo mengi lakini unasema na kuna Dar es Salaam, tayari kuna Banana unatka uje na fourth generation meli ambazo ni kubwa zinashusha zinapakia wenyewe haziwezi tena kuingia Dar es Salaam, pengine kina cha bandari cha Dar es Salaam kitagoma kupokea meli hizo za fourth generation na tukaenda itakuja fifth na sixth generation. Meli moja ya sasa inaweza kuwa na tani milioni 100 inaleta mzigo wa tani pengine milioni mbili, pengine Dar es Salaam isiweze kubeba tena. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa pale Dar es Salaam pameshajaa...

SPIKA: Mheshimiwa Ally Saleh bahati mbaya dakika saba zimeisha.