Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niseme machache katika Wizara hii kwanza niwapongeze Mheshimiwa Waziri na timu yako kwa jinsi ambavyo wanaipeleka Wizara hii iweze kusonga mbele. Piai niwape hongera sana hasa kwa kazi wanayofanya kwa ATCL wamekuwa na vituo tisa katika nchi lakini vitano katika kanda hongereni sana. Vile vile wamekuwa na destinations tano nje ya Nchi za Rwanda, Burundi, Zimbabwe, Zambia, Comoro, lakini mna matarajio ya destinations katika nchi tano Thailand, India, Afrika Kusini na China na haya wanayatekeleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, niwapongeze pia kwa sababu sasa wana mpango wa kuongeza ndege mbili tena dreamliner na bombardier tena ambazo zitaingia mapema mwakani hongereni sana. Pia wanafanya kazi kubwa ya kuwafundisha Marubani wetu 51, Wahudumu 66, Wahandisi 14, lakini abiria wameongeza kutoka 200,000 mpaka 300,000, hongereni sana. Naomba wasikate tama, hii kazi ni kubwa na wameitambulisha nchi yetu katika nchi zingine, jambo ambalo lilikuwa halijawahi kufanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri, nimekuwa nikiongea kuhusu bypass ya Babati kutoka Arusha kuja Dodoma na Singida, sasa nimeona bilioni ambazo ametutengea kwa ajili ya fidia ya wale wananchi wa Babati, Mruki, Hangoni, Sigino na hii bypass inakwenda kutekelezwa, jambo ambalo lilikuwa halijawahi kufanyika hongereni sana na tunashukuru. Pia niwaombe kuhusu suala zima la uwanja wa ndege katika Mkoa wetu wa Manyara. Mheshimiwa Waziri Mkoa wa Manyara hatuna uwanja wa ndege, tumesema sana muda mrefu sana tunaomba watuwekee hata kwa changarawe, sio lazima lami kwa sasa, naomba hili walichukue kwa sababu mengi tumekuwa tukiyasema na wamekuwa wakiyachukua, naamini na hili pia watalichukua.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimwombe Mheshimiwa Waziri suala la malipo ya fidia kwa wale ambao mita za barabara zimeongezeka sasa, nimekuwa nikisema kwamba tunahitaji kuwafidia wale ambao nyumba zao sasa zimeathirika na zile reserve. Ni vizuri wakaliangalia hili kwa sababu neema tuliyoipata ya Babati kuunganishwa na barabara Singida-Arusha-Dodoma pia imezaa hili linguine, naamini watalifanyia kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu watu wa TBA wako nao siku ya leo niwaombe pia maeneo ya National Housing yamekabidhiwa kwa TBA pale mjini, Mheshimiwa Waziri nilishamjulisha hili tunahitaji eneo la pale mjini kwa ajili ya matumizi ya halmashauri sasa na kuwapanga vijana wetu wale Wamachinga ambao wanahitaji kutumia eneo hilo naamini na hili watatupatia pia.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa ufupi pia barabara yetu ile inayoanzia Singe nishukuru wameiweka na inaendelea na ujenzi kila mwaka kwenda Kiteto, ni vizuri sasa wakatuongezea fedha kwa sababu itatupunguzia kilomita zaidi ya 78 kuja Dodoma. Sasa kwa sababu hii imekamilika ya Kondoa- Babati naamini hii ya Singe, Sukulo na maeneo mengine inaweza ikaturahisishia sana watu wa Babati kuelekea Dar es Salaam, hii barabara wakiikamilsha kwa kiwango cha lami jambo linaendelea sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia niwaombe barabara ya Dareda-Dongobeshi kuelekea Hospitali ya Rufaa ya Hydom wamekuwa wakiweka, nashukuru pia wameweka hata mwaka huu, lakini sasa ni vizuri tukafikiria kuunganisha na hii inayotoka Karatu kuelekea Mbulu na Singida kwa kiwango cha lami. Nishukuru hiyo ya Karatu - Mbulu, Hydom - Singida mmeshai-cover lakini sasa hii ya Babati – Dareda – Dongobeshi - Hydom Mheshimiwa Waziri wakiweka pia itatusaidia sana. Otherwise wanafanya kazi nzuri hongereni na niwapongeze wamepokea zaidi ya asilimia 60 ya bajeti, nipongeze Wizara ya Fedha na Wizara yao na wanachapa kazi. Pia niwapongeze kwa kuwa wazalendo wameona kwamba wawe na bajeti ambayo inatekelezeka zaidi ya trilioni mbili mpaka 1.5.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja na ahsante. (Makofi)