Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushuru kwanza kabisa nichukue fursa hii kuipongeza Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Jemedari makini kabisa Dkt. John Pombe Magufuli, kwa kazi nzuri sana ambayo imeendelea kuifanya na ama kwa hakika watanzania tunaona mwanga mbele kule kwamba tunaona tunaenda kuipata tanzania mpya. Na tanzania mpya kweli inawezekana chini ya Dkt. Magufuli.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia nimpongeze Mheshimiwa Waziri na Manaibu wake wote wawili ndugu yangu Mheshimiwa Kwandikwa na na mwenzangu Mheshimiwa Engineer Nditiye nimpongeze katibu Mkuu wa Wizara hii architecture mwenzangu Mwakalinga lakini pamoja na watendaji wote pamoja na wakuu wa taasisi zote zilizopo chini ya Wizara hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na pongezi zote hizo kwa kazi inayoendelea naomba nichangie mambo machache kama ifuatavyo:-

Kwanza kabisa nitapenda kuongelea barabara yetu ya kutoka Dodoma kwenda Babati ambayo inapita pale kwangu Kondoa Mjini ni barabara nzuri na ya viwango ambavyo havina shaka wakati mwingine unaweza kuendesha mpaka unaweka ile cruise control sina hakika katika nchi ya Tanzania ama na sehemu nyingine barabara nzuri kama ile unaipata wapi nawapongeza sana kwa viwango vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo karibu kidogo naunafika kondoa mjini lipo daraja moja linaitwa Msangalale. Daraja lile limekaa sehemu ambayo kama inamtego kidogo kuna mlima halafu kuna kona kunamteremko wa hatari sana kumekuwa kukisabisha ajali nyingi, watu wamekufa, watu wengi sana wamepoteza maisha pale na wengine wamepata vilema. Sasa niliwahi kuzungumza siku moja kwenye RCC na ninamshukuru sana Engineer wa Mkoa wa Dodoma Eng.Leonard Chimagu alili-react haraka na wakafanya utaratibu wakweka alama za hatari lakini pia wakweka tuta la kupunguza speed.

Mheshimiwa Naibu Spika, bahati mbaya eneo lilipowekwa lile tuta na eneo ilipowekwa ile alama ni karibu sana na lile daraja matokeo yake bado ajali zimeendelea nakuja mtu huko na spidi yake kwa sababu barabara ipo tamu, anakuja na speed yake anaona alama hii hapa ghafla tuta, na tuta lenyewe bahati mbaya pia halina ubora wa sahihi ukiligonga lile watu wanarukia mtoni. Mara kadhaa malori yamedondoka na mara kadhaa gari ndogo zimedonga na zimesabisha kupoteza maisha kwa wapita njia pale. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Sasa basi ushauri wangu ni nini, alama zisogeze nyuma na ninaomba sana Wizara ilizingatie na kulifuatilia hili, alama isogezwe nyumba na lile bampu lilekebishwe vile viwango vyake vilivyoweka lisiwe la kustukiza wakati mwingine linaharibu hata gari. Halafu kabla ya bampu huwa kunakuwa wanaita kama rasta hivi zisogee nyuma kidogo takribani viwango ninyi mnavijua na ninaamini suala hili kadri nilivyolieleza mtaweza kulirekebisha kwa upande kama unatoka Dodoma na kwa upande kama unatoka Kondoa sehemu zote mbili alama za hatari ziwekwe mbali ile kona imekaa vibaya sana hilo ni moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo la pili kwa upande wa barabara nataka niongelee barabara inaoyounganisha Kondoa kwenda mpaka Kateshi mmtenga bilioni 50 kwa ajili ya barabara ya Munguri lakini hapa Kondoa Mjini lipo daraja la mto mkondoa si daraja kuna daraja dogo ambalo sio la barabara ya TANROADS maximum ni tani 10 malori makubwa hayawezi kupita ili barabara ile ya TANROADS maroli makubwa yapite yanapita korongoni. Sasa napo pale lazima kuweka daraja kwa sababu kunganisha usafiri kati ya kondoa mpaka Kateshi lile daraja la Mto Mkondoa la lenyewe lazima lifanyiwe kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana hilo mlingalie vinginevyo magari yatakuwa yanapita halafu yanakwamia pale kwenye Mto Mkondoa. Ukitaka kupitia hili daraja hili la tani 10 malori makubwa hayawezi kupita halafu inaingia mjini kuna kona dongo sana malori makubwa hajawezi kupita naomba sana hilo liangaliwe hilo ni jambo la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili Jimbo la Kondoa lipo mjini kabisa lakini bado tunazo kata kama sita hivi suala la masiliano ni changomoto kubwa tunazungumzia Kata ya Kingare. Mheshimiwa Naibu Waziri Engineer Nditiye niliwahi kukugusia hii na orodha nilikupa Kata kingare maeneo ya Kampori na mengineyo tunazungumzia Kata ya Suruke, tunazungumziea Kata ya Seria maeneo ya Hurumbi na Dumu na Chandimo tunazungumzia Kata ya Koro maeneo ya Chora na Hachwi, tunazungumzia Kata ya Borisa, tunazungumzia na Kata ya Kondoa Mjini yenyewe hebu fikiria mjini kwenye kuna maeneo ya Tumbero na Chang’ombe hakuna mawasiliano.

Mheshimiwa Naibu Spika, hili nakuomba sana Mheshimiwa Naibu Waziri hebu lifanyie kazi pale mjini tujisikie nasi tunaweza kupata huduma muhimu vinginevyo sisi tupo Makao Makuu, kweli tupo Makao Makuu halafu tunakosa mawasiliano jamani. Jiji la Dodoma Makao Makuu ya nchi hebu naomba tusaidie sana kwenye hili nilitamani sana niseme zaidi lakini naona kama dakika zangu umenipa mbili sijui…(Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)