Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia Wizara hii. Nina mambo mawili tu ya kuchangia.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza ni mambo ya jimboni; napenda nitoe shukrani za dhati kwa Mamlaka ya Bandari Tanzania kwa miradi ambayo imeanza kuifanya katika Mkoa wa Kigoma katika Manispaa ya Kigoma Ujiji, Bandari ya Ujiji, Bandari ya Kibirizi na Bandari ya Nchi Kavu ya Katosho. Bandari ya Nchi Kavu ya Katosho umuhimu wake ni kuhakikisha kwamba Kigoma inakuwa ni kituo cha biashara kama ambavyo imekuwa siku zote kwamba eneo la Ujiji na Kigoma ni eneo la biashara la Maziwa Makuu na hivyo kuwezesha mizigo ambayo inatoka Bandari ya Dar es Salaam kwenda Burundi au kwenda Mashariki ya Congo upande wa Kaskazini ya Mashariki ya Congo watu waweze kuichukua pale Kigoma, kuifanya Kigoma ni plot of destination. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo Mamlaka ya Bandari kwa kazi hizi ambazo wanaendelea kuzifanya na maeneo mengine nimeona bajeti wamepanga ya shilingi bilioni 548 kwa ajili ya miradi mbalimbali ya Mamlaka ya Bandari nchi nzima, ni kazi ambayo ni nzuri kwa sababu maendeleo yake yanaendana na maendeleo ya jumla. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, niombe Wizara itupatie majibu ni kwa nini kama jinsi alivyoongea Mheshimiwa Nsanzugwanko jana, ni kwa nini Mradi wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma unazidi kucheleshwa? Tunafahamu kwamba manunuzi yameshakamilika toka mwezi Januari, 2018, sasa hivi ni mwezi Mei, 2019, hatujaona chochote ambacho kinafanyika katika Uwanja wa Ndege wa Kigoma, viwanja vingine tunaona vikijengwa, vingine vipya havikuwepo kabisa vinajengwa, kwa nini mradi ambao tayari una fedha kutoka European Investment Bank unaendelea kucheleweshwa mpaka sasa hivi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine, tuna mradi mkubwa sana wa takribani dola milioni 40 wa upanuzi wa Bandari ya Kigoma ambao unafadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Japan (JICA). Juzi niliona Mheshimiwa Waziri wa Fedha akiwa amezungumza na watu wa JICA alivyokuwa kule Washington, lakini mpaka sasa hatujaona taarifa yoyote ile kuhusiana na mradi huu wa Kigoma. Nilivyofuatilia niliambiwa kwamba kuna masuala ya kikodi na kadhalika, nadhani kuna haja ya Serikali kuweza kuona vitu ambavyo msaada huu kutoka Japan wanaomba viingie bila kulipia kodi kama faida yake ni kubwa kuliko mradi wenyewe kwa ujumla wake, kwa sababu kuingiza dola milioni 40 katika Mji wa Kigoma kwa ajili ya ujenzi wa Bandari ya Kigoma nadhani una faida kubwa zaidi kuliko VAT ambayo wanaomba iwe exempted kwa ajili ya kuingiza vifaa vyao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo naamini kabisa kwamba Wizara na hasa Wizara ya Fedha na Mheshimiwa Waziri Mpango yupo hapa, watahakikisha jambo hili linakamilika sababu mwezi huu Mei ulitakiwa mradi uwe umeanza, mpaka sasa Wizara ya Fedha bado haijasaini mkataba na JICA kwa ajili ya mradi huu, zabuni zitangazwe ili uweze kuanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa lingine ni suala la kinchi la kiujumla. Mheshimiwa Silinde amezungumza hapa, toka tumeanza Awamu ya Tano fedha ambazo tumeziingiza Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi ni asilimia 46 ya bajeti yote ya maendeleo ya nchi yetu. Jumla ya fedha ambazo tumeziingiza Wizara hii ni trilioni 18.7 na fedha ambazo za ujumla za bajeti ya maendeleo ya nchi ni trilioni 40.6. Kwa hiyo 46 percent ya bajeti ya maendeleo anaishika Mheshimiwa Kamwelwe na Manaibu wake wawili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Wabunge wana haki ya kuuliza kiasi hiki cha fedha ambacho tumekiingiza mpaka sasa kimezalisha viwanda vingapi? Kwa sababu tunazungumza kuhusu forward and backward linkages, tunazungumza kuhusu namna gani ambavyo fedha tunazoziingiza kwenye miradi kama reli, miradi kama ndege ni namna gani ambazo zinachochea sekta nyingine za uchumi. Kwa hiyo, tungepata maelezo ya Serikali hapa kwamba tumeingiza trilioni 18.7, nini multiplier effect ya hili na Mheshimiwa Waziri Mpango analijua vizuri sana. Moja ya sekta ambayo ina-multiplier effect kubwa ni construction sekta. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini sisi ambao tunaingiza fedha nyingi namna hii bado kasi ya ukuaji wa uchumi iwe ni ndogo, leo hii tunabishania makisio ambayo haya IMF wameyatoa ya four percent na kadhalika, IMF Mheshimiwa Waziri Mpango hawajakanusha kuhusu makisio hayo, wamekanusha ripped report lakini makisio ni yale yale, lakini hata usipochukua makisio ya IMF chukua makisio ya Serikali ya six percent before Serikali ya Awamu ya Tano kuingia madarakani economy yetu ilikuwa inakua kwa seven percent for 10 years. Serikali ya Awamu ya Tano imeingia madarakani 18 trillion shillings zimeingizwa kwenye construction sector, growth rate iko chini kwa nini? Haya ndio masuala ambayo Wabunge tunapaswa kuiuliza Serikali, (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Kenya wamejenga ile SGR ya mkopo wenyewe ghari sana na wote tunajua, lakini mchango wa ujenzi building construction kwenye growth rate ilikuwa 1.5 percent, iweje sisi warithi growth rate ya seven percent halafu ndani ya miaka mitatu baada ya ku-inject all the money tushuke, nimesema waachane na four percent ya IMF, waende na six percent ya Serikali, why? Ni kwa sababu utekelezaji wetu wa mipango ya maendeleo ya miundombinu ni utekelezaji unaotoa fedha kwenda nje, hauingizi ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ndio maana mzunguko wa fedha ni mdogo sana kwa sababu wamewapa kazi wakandarasi wa nje, wanaagiza raw materials kutoka nje, every single cent amount ya nchi yetu inapelekwa nje, wanakusanya kodi kwa muuza nyanya, wanaenda kumlipa Mturuki anapeleka Uturuki, ndio maana uchumi haukui. Hata wajenge argument namna gani. Nimeona argument ya Serikali kwenda IMF kusema makisio haya ni makosa kwa sababu tuna miradi mikubwa, tuna SGR, tuna sijui Stiegler’s Gorge, argument ile haina maana kwa sababu all the money zinaenda nje na debt service yetu, huduma yetu ya Deni la Taifa ni kubwa...(Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Zitto kuna taarifa hapo, Mheshimiwa Waziri wa Fedha.

T A A R I F A

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Naibu Spika, naipokea taarifa ya Mheshimiwa Waziri Mpango. Ninachotaka kumwambia Mheshimiwa Waziri Mpango kwanza anajua kwamba mamlaka ya economic surveillance ya dunia ni moja, ni IMF na anafahamu kwa sababu amefanya kazi huko, Benki ya Dunia, African Development Bank na hata Wizara yetu ya Fedha makisio wanayoyatumia ni makisio ya IMF, sio makisio mengine yoyote na anafahamu, labda atakataa kwa sababu lazima a-defend Serikali hapa, lakini najua anafahamu hivyo. Hata hivyo, point yangu ni kwamba, wastani wa over a decade thus why tulikuwa sisi ni the fastest growing economy, wastani wa over a decade ni seven percent, sawa we can debate about that... (Makofi)

NAIBU SPIKA: Nashauri Waheshimiwa Wabunge ongeeni huku ili iwarahisishie kwenda na mazungumzo mnayotaka kuzungumza, mkianza kutazama wenyewe huko ndio hayo mnaanza kujibizana wenyewe, zungumza na mimi huku ili usipate wakati mgumu kuona mtu amekataa jambo lako.

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Naomba nichukue takwimu za Mheshimiwa Waziri Mpango, yeye ni mchumi anajua, panapokuwa na depression, panapokuwa na mdororo wote wa uchumi kwa kutumia fiscal Policy Serikali ina-pump in money kwa ajili ya kuchochea uchumi, over the last three years, tume-pump 18.7 trillion kwenye construction. Naomba nijibiwe, hii fedha ambayo tumei-pump tumezalisha viwanda vingapi, tumezalisha ajira za kudumu ngapi, sekta ya kilimo imechochewa namna gani, ndio maana ya multiplier effect na ndio swali langu hili na wakati mwingine tunapozungumza wala hatuna nia mbaya, nia yetu ni kuhakikisha kwamba tunakwenda pamoja as a country, hakuna mtu ambaye hataki nchi yake iendelee, so there is no haja ya kuwa defensive. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukweli ni kwamba utekelezaji wa sera za kiuchumi wa nchi yetu over the last four years ni utekelezaji mbovu, ni utekelezaji fyongo, ndio maana pumping in of money, 20 percent ya development budget tunayoiingiza, haichochei uchumi inavyotakiwa.

T A A R I F A

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Naibu Spika, sipokei taarifa ya dada yangu na namtakia mfungo mwema wa mwezi wa Ramadhani na ajiepushe sana kutumia maneno kupotosha kwa sababu mimi siwezi kutumia hayo dhidi yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna tofauti kubwa sana kati ya kasi ya ukuaji wa uchumi na uchumi. Sekta ya ujenzi ni ya pili kwenye kasi ya ukuaji, sio ya pili kwenye uchangiaji wa uchumi. Sekta ya ujenzi inachangia kidogo sana kwenye uchumi, ni ya pili kwenye ukuaji, we have to pump in all this money, lakini huo wa pili wake hauonekani kwenye uchumi wa ujumla wake na ndio argument yangu, kwamba almost half mama ya development budget.(Makofi)

NAIBU SPIKA: Ongea na kiti mwache Mheshimiwa Dkt. Ashatu.

MHE KABWE. Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Naibu Spika, nusu ya fedha zako za maendeleo unaziingiza kwenye sekta moja, Wizara moja unapaswa uone namna ambavyo sekta zingine zimeinuliwa na ndio maana maswali hapa nimeuliza. Serikali ije kutujibu hii investment ambayo tumefanya imezalisha viwanda vingapi?

Mheshimiwa Naibu Spika, construction sector impact yake sio long term inaanza na short term, mfano mzuri, anaweza akawa ni kijana anatengeneza screw za ujenzi wa reli, akapata kazi, screw tu ni moja ya kiwanda ambacho kinaweza kikatengeneza wakati huo na akiendelea maana yake wawe wamefanya transfer of technology, wameajiri, wame-train ataendelea na ile kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninachokiomba, muundo wetu wa mipango ya kiuchumi na utekelezaji wa miradi yetu iangalie backward and forwarding linkages ili fedha ambayo tunaiingiza public investment ambayo tunaifanya iweze kuwa na faida zaidi kwa nchi yetu kwa ujumla wake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimalizie mambo mawili…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)