Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia, nimpongeze Abbas alivyokuwa anachangia hapa vizuri zaidi amenikumbusha uwezo wa kawaida wa binadamu wa kufikiri ule unaitwa argue ni 100 na inaenda mpaka 150. Lakini wale wataalam wenye akili nyingi zaidi kama Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli wanaanza 170 mpaka 220 argue. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tofauti yetu tulio wengi hapa Bungeni na Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli ni moja tu yeye IQ yake kwa kuwa ni kubwa anawaza Tanzania ya 2050 itakuwaje wakati huo huo sisi tunawaza lini tunakuja Bungeni kuendelea na maisha yetu ndiyo tofauti yetu. Kama unawaza kurudi Bungeni unaweza ukazungumza vitu rahisi rahisi vya kufurahisha watu ili uje Bungeni hapa kama unawaza nchi itakavyokuwa huko mbele maana yake ni kwamba unawaza mambo makubwa bila kujali itakuwaje, waanguke au usianguke, ndiyo Mheshimiw Rais Dkt. John Pombe Magufuli anafanya mambo kama hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimeshangaa kuna vitu vingine hapa vinakuwa kama mtu anakuja vibaya, au anakuja vizuri sasa tunaambiwa bwana nyie wa CCM sijui Wabunge tunawapa ushauri hamfuati, ushauri siyo agizo, ushauri kuna ushauri mzuri kuna good advice na kuna bad advice. Kwa hiyo, ushauri unaweza ukaufuata kama unaona kama unakufaa au haukufai, ndiyo maana unaitwa ushauri. Tungefuata ushauri huo basi kulikuwa na lugha hapa mnajenga ndege za nini mnajenga reli za nini bandari sijui yameenda, lakini leo tunashauriwa leo nimeona hapa Mheshimiwa Silinde anashauri juu ya kuendeleza mapato ya ndege.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo ina maana amekubali ndege ni sahihi kuletwa hapa nchini. Kwa hiyo, tunakubaliana, leo tumeona watu wanashauri kujenga bandari kavu, ambayo bandari kavu kuijenga ni miezi mitatu, lakini kujenga reli ni zaidi ya mwaka mmoja miaka miwili. Kwa hiyo, tumeanza kile kikubwa tunakuja kwenye kile kidogo ili tuweze kwenda vizuri kwenye mambo yetu tunayoenda. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niende kwenye barabara za Jimbo la Bunda na kwenye barabara za Mkoa wa Mara. Kuna barabara ya kutoka Nyamswa kwenda Bunda, Bunda kwenda Buramba, Buramba kwenda Kisolia, kuna barabara hiyo ipo toka mwaka 2000 mpaka leo haijajengwa amekuja Mheshimiwa Rais tarehe 4 alikuwa Kibara mwezi wa 9 tarehe 6 alikuwa kwenye Jimbo la Bunda ameagiza amefungua ujenzi wa hiyo barabara akaagiza nikitoka hapa kasi ya barabara hii iendelee.

Mheshimiwa Naibu Spika, mpaka sasa ni miezi 9 sasa barabara hii haiendi, barabara ya Buramba kwenda Kisolia haiendi, barabara ya Nyamswa kuja Bunda haijatangwaza hata mkandarasi hajapitiaka, barabara ya makutano kule Sanzati bado inasuasua haiku vizuri, barabara ya kutoka Sangati kwenda Natamgumu bado iko vibaya. Sasa najiuliza sasa Wizara hii ya ujenzi na miundombinu kama kuna mtu alioa Mara halafu mke akamkimbia aje tumrudishie sasa shida iko wapi? Mbona sisi tunapata shida? Ukienda kwenye uwanja wa ndege tumeahidiwa mpaka leo haupo ukienda kwenye bandari haipo sasa ni nini kinatokea sasa kwenye Mkoa wa Mara kitu gani kinakuwepo? Tuna hasira sasa na mambo kama haya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba sasa Wizara ianze kuona Mheshimiwa Rais ametoa agizo la kujenga barabara hizo na kutangaza wakandarasi shida yetu iko wapi. Kweli tukafikiri kwamba watu waweze kujenga ili tuweze kuona kazi inaenda. Lakini vinginevyo uwanja wa ndege wa Musoma umepewa bilioni 10 na hautatolewa mpaka leo haujatolewa, Wizara hii ya Ujenzi kusema kweli nchi ni kubwa na wanafanya kazi nzuri niwapongeze kusema kweli, Mheshimiwa Engineer Kamwelwe naomba sasa naomba sasa ujitahidi ufanye kazi vizuri, Mheshimiwa Engineer Nditiye umsaidie Mheshimiwa Kwandika nawe umsaidie na watendaji wote wa Wizara hii msaidiane nchi ni kubwa tusipoangalia sasa namna ya kupanga hivi vipande vyetu na keki yetu maeneo mengine yatakufa, yataendelea kupata shida sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tuangalie kuangalia Mkoa wa Mara muuangalie, Mheshimiwa Rais ameusemea sana alipokuwa kule ndani na mwaka huu tuna maazimisho ya Mwalimu mwezi wa 10 tunataka zile barabara zipitike ili wageni watakavyokuja pale kutoka South Africa wawepo.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Muda wako umeesha Mheshimiwa, kengele imeshagonga, ahsante sana.

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, dakika tatu hamna? (Vicheko)