Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Peter Ambrose Lijualikali

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kilombero

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. PETER A. LIJUALIKALI: Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Kilombero haina Hospitali ya Wilaya, Hospitali inayotumika ni Mtakatifu Fransisco lakini gharama zake ni kubwa kidogo kwa watu wengi kuweza kumudu.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia tuna Vituo vya Afya vya Kibaoni, Mang’ula na Kidatu. Vituo hivi havikidhi mahitaji ya kihuduma na tiba.

Mheshimiwa Naibu Spika, watu wa Kilombero ni zaidi ya 500,000. Bila ya kupata Hospitali ya Wilaya, bado bituo hivi vitakuwa na kazi kubwa hivyo kupunguza ufanisi. Tunaomba kupatiwa Hospitali ya Wilaya ya Kilombero.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.