Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nitoe pongezi zangu kwa Serikali ya Awamu ya Tano, pia kwake Mheshimiwa Waziri Ummy na Naibu wake, Mheshimiwa Dkt. F. Ndugulile, kwa kufanya kazi kwa weledi mkubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na shukrani hizi, naomba nikumbushe jambo moja kwamba Dongobesh, Kituo cha Afya na Jimbo la Mbulu Vijijini hatuna kabisa gari la wagonjwa (ambulance) la kuwahudumia wananchi. Pia Mheshimiwa Ummy akumbuke ilikuwa ahadi yake pale Dongobesh baada ya ziara yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, kweli nakubali kazi wanayofanya Mheshimiwa Ummy na Naibu Waziri, Mheshimiwa Dkt. Faustine, wamefanya ziara ya kuona changamoto za Mbulu Vijijini. Pia tumejengewa kituo kimoja cha afya cha Dongobesh, ahsanteni sana. Hospitali ya Halimashauri ya Wilaya inajengwa, ahsante.

Mheshimiwa Naibu Spika, nawaombea Mungu warudi tena katika nafasi zao baada ya mwaka 2020 katika Uchaguzi Mkuu. Mungu atujalie, ahsanteni.