Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali nawapongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa kazi nzuri wanayoendelea kuifanya katika Sekta hii muhimu sana kwa maisha ya mwanadamu. Nawapongeza pia Katibu Mkuu, viongozi na watumishi wote wa Wizara kwa bajeti nzuri na kwa kuchapa kazi. Mwenyezi Mungu aendelee kuwawezesha.

Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Serikali kwa maboresho makubwa katika Sekta ya Afya nchi nzima. Hii ni kazi kubwa sana na ni ukombozi kwa wananchi wa Tanzania. Kufungamananisha uchumi na maendeleo ya wananchi kunaonekana katika sekta hii. Sasa naiomba Serikali yangu ilete Muswada Bungeni wa Sheria ya Bima ya Afya kwa wote ili wananchi wafaidike na huduma bora za afya nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, naishukuru Serikali kwa kulipatia Jimbo langu zaidi ya shilingi bilioni moja kujenga vituo vya afya viwili na kuvipatia vifaa tiba. Vituo hivyo ni Kerege na Matimbwa. Vituo hivi vitachangia sana kuboresha huduma ya afya Bagamoyo. Kituo cha Afya Kerege kimeanza kufanya kazi isipokuwa cha Matimbwa (Yombo) bado hakijaanza kazi. Namwomba Mheshimiwa Waziri atusaidie kupata samani, vifaa tiba na watumishi wa ajili ya Kituo cha Afya cha Matimbwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji zaidi ya 20 (kata tano) katika barabara ya Bagamoyo Msata (kilometa 64) havina huduma ya kituo cha afya. Namwomba Mheshimiwa Waziri atupangie kituo cha afya katika eneo hilo kubwa toka Bagamoyo mpaka Msata.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.