Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Serikali kuongeza watendaji katika Sekta ya Afya, kwani Madaktari ni wachache, hivyo wanazidiwa na kazi, wanachoka na hivyo kufanya kazi chini ya kiwango.

Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Wizara hii kuhakikisha inatoa elimu juu ya afya za Watanzania badala ya kusubiri waugue ndipo wawaelimishe. Pia Wizara ya Afya itoe kinga nyingi ili kupunguza gharama za matibabu. Naishauri Serikali kutoa ufadhili kwenye magonjwa yasiyoambukiza, kwa mfano, kisukari kinawapata watu ambao uwezo wao wa kutafuta fedha za kujitibia hawana, hivyo, wazee hawa wanakufa kabla ya muda.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaendelea kuishauri serikali kuwa wagonjwa wa UKIMWI hawafi kwa kutotumia ARV bali wanakufa kwa magonjwa kama Kifua Kikuu, kuharisha na typhoid. Hivyo tunashauri kwenye ARV ziwepo ceptrine ili pale mgonjwa anapopata magonjwa nyemelezi waweze kupewa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nyongeza ya Madaktari wa upasuaji katika Hospitali ya Tumbi kwani hospitali hii inapokea wagonjwa wa ajali za barabara ya Morogoro. Wawili waliopo hawatoshi, tuongezewe, kwani hospitali hii imepandishwa hadhi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Bima ya Afya imeonesha kasoro nyingi ikiwepo usumbufu wa kutopata huduma stahiki, mfano dawa mara nyingine uambiwe ukanunue au mara nyingine uambiwe ni kwa magonjwa baadhi tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba wahudumu wa afya msingi waajiriwe ili kusaidia huduma za vijijini. Wahudumu hawa walikuwa msaada sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, matibabu kwa wazee ni shida. Bima walizoahidiwa hawajapewa na waliopewa hawapati huduma hizo hospitalini.