Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Catherine Nyakao Ruge

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. CATHERINE N. RUGE: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuchangia mambo machache katika Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto. Kwanza nianze na suala la uzazi wa mpango. Kuna msemo unasema if you fail to plan you have planned to fail. Ongezeko la watu katika nchi yetu limekuwa likiongezeka kwa asilimia 27 katika nchi yetu. Tanzania inakadiriwa kuwa na watu milioni 150 ifikapo mwaka 2050. Je, kama nchi tumejiandaa kuhudumia ongezeko hilo la watu ukizingatia ongezeko hilo la watu na limited resources tulizonazo?

Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu dhana ya Serikali ya kuongeza matumizi ya njia za kisasa za uzazi wa mpango kutoka 32% - 45% ifikapo mwaka 2020, pia kupunguza vifo vya akina mama wakati wa kujifungua kutoka vifo 556 - 292 kwa vizazi hadi vifo 100,000, ifikapo mwaka 2020; kupunguza mimba za utotoni toka 27% - 22% ifikapo 2020. Naomba majibu ya Serikali, sasa hivi tumefikia wapi katika malengo tajwa hapo juu ikiwa tumebakiza mwaka mmoja tu kufika mwaka 2020?

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda pia kuzungumzia suala la Community Health Workers (CHWs)au watoa huduma za afya ngazi ya jamii wamekuwa na mchango mkubwa sana katika kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na watoto chini ya miaka mitano. CHWs wamekuwa wakitoa elimu kuhusu lishe ya watoto, akina mama wajawazito na kuhamasisha akina mama wajawazito kwenda kujifungulia katika vituo vua afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, mfano hai ni Kijiji cha Uturo Mbarali hakijaripoti kifo cha akina mama kwa zaidi ya miaka mitano kwa sababu wamekuwa wakiwatumia CHWs katika jamii. Nafahamu mpango mkakati wa IV wa Wizara ya Afya umetambua kada hii na umeonesha kwamba mpaka mwaka 2020 itakuwa imeajiri CHWs 5000, lakini mpaka sasa Serikali haijaajiri hata CHW mmoja licha ya service scheme kukamilika mwaka 2018, Desemba.

Mheshimiwa Naibu Spika, Global Funds walitoa pesa kwa ajili ya motisha kwa CHWs na mradi huu unakamilika mwaka 2020, lakini Serikali imegoma kuwatumia CHWs kwa pesa za Global Funds.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Waziri akija kuhitimisha anijibu maswali yafuatayo:-

(a) Ni lini Serikali itaajiri CHWs kama ilivyoahidi kwenye mkakati wa IV wa Wizara ya Afya?

(b) Pesa zilizotolewa na Global Funds ziko wapi?

(c) Kwa nini Halmashauri zinazotaka kuajiri CHWs kwa makato yao ya ndani zinakatazwa kuajiri?

(d) Ni nini mkakati wa Serikali kupunguza vifo vya akina mama wajawazito hasa wanaojifungulia majumbani ikiwa Serikali haitaki kufanya kazi na kuwatambua CHWs?

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.