Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Kiteto Zawadi Koshuma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. KITETO Z. KOSHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kupitia taasisi mbalimbali zinazotoa matibabu ya kibingwa. Pia nawapongeza Waheshimiwa Mawaziri wa Wizara ya Afya kwa ushirikiano wao kwa Waheshimiwa Wabunge katika kuhudumia wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu afya ya uzazi, mama na mtoto; Serikali imejitahidi sana kujenga zahanati na vituo vya afya na hivyo kupunguza mwendo mrefu wa wananchi pamoja na kinamama wajawazito ili kufikia huduma za afya, lakini bado vifo vya mama na mtoto idadi ipo juu hususan akina mama wajawazito ambapo takwimu zinaonesha kuwa akina mama 24 wanafariki kila siku wanapokuwa wanajifungua.

Mheshimiwa Naibu Spika, vifo vingi hutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kutokwa na damu nyingi wakati wa kujifungua, kutokufanya maamuzi ya njia za kujifungua mapema kama vile upasuaji, ukosefu wa dawa aina ya misoprostol and oxytocin hususan vijijini na pia ukosefu wa vifaa tiba na wataalam wa kutosha katika vituo vya afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, suluhisho ni kwamba Serikali iweke mkakati wa kuajiri Community Health Workers na wasambazwe maeneo yote hususan katika zahanati na vituo vya afya vya vijijini ili waweze kutoa huduma za afya na elimu kwa akina mama wajawazito. Ni vyema Serikali itenge fedha kwa ajili ya kukabiliana na vifo vya mama na mtoto.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho kabisa, naomba Serikali iharakishe mchakato wa kuleta sheria ya Universal Health Coverage ili kuwezesha wananchi wote wapate huduma bora za afya kwa usawa. Pia Serikali ijitahidi kutafuta wafadhili ili kusambaza vifaa kwa ajili ya kuanzia kusajili wananchi na huduma ya NHIF iliyoboreshwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.