Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Katani Ahmadi Katani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tandahimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. KATANI A. KATANI: Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Tandahimba ina hospitali moja ya Wilaya na vitu viwili vya afya ambavyo ni vya zamani. Hata hivyo, tunaishukuru Serikali kwa kutupatia fedha shilingi milioni 400 za Tanzania kwa ajili ya ukarabati wa Kituo cha Afya Mahuta. Fedha hizi zimetumika vizuri. Kwa hiyo, ombi langu ni kupata fedha kwa ajili ya ukarabati na upanuzi wa kituo hiki ambacho kinahudumia zaidi ya kata kumi zilizopo jirani. Hata hivyo, Wilaya ya Tandahimba jiografia yake ni ngumu kidogo, kwa hiyo, naomba Wizara itusaidie fedha kwa ajili ya kujenga na kuendeleza vituo vya afya vipya vilivyojengwa na wananchi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Kata ya Mnyawa wananchi kwa kupenda maendeleo wamejenga vituo vya afya ambavyo vinahitaji msaada wa Serikali ili tuweze kumalizia. Kata ya Mndumbwe nayo wananchi wamejitolea kujenga kituo cha afya. Tunaomba msaada kwa Serikali iweze kutusaidia tumalize ujenzi huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba Wizara itujengee Kituo cha Afya katika Tarafa ya Litehu ambayo inahudumia wakazi zaidi ya 30,000. Tunaomba tupate kituo cha afya katika Kata ya Kitama I. Kituo ambacho kitasaidia kuboresha huduma za afya katika maeneo jirani kama Kata ya Miute, Michenjele, Mihambwe na Mkoreha. Wananchi wako tayari kujitolea, nami kama mwakilishi wa Jimbo la Tandahimba na mzaliwa wa Kitama, naahidi kuchangia mifuko 600 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho. Kwa unyenyekevu mkubwa naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante naomba kuwasilisha.