Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE: Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia njia ya maandishi nichangie bajeti ya Wizara ya Afya. Awali ya yote nichukue fursa hi kuunga mkono hoja bajeti hii na niwapongeze viongozi na watendaji wote wa Wizara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kuishauri Wizara iweze kupitia upya upangaji wa watendaji maalum katika wizara hii ili angalau kila mkoa upate hao wataalamu wa msingi. Mfano, mwezi wa tatu Mkoa wa Kagera kwa hospitali zote Umma na binafsi hakukuwepo Mganga kwa ajili ya magonjwa ya akina mama (gynocologist). Hoja hapa ni kuhakikisha kila mkoa unapata wataalamu hawa na hata wakati wa kutoa ajira muhimu, kutoa nafasi kwa utaratibu huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kupitia bajeti hii, nishauri juu ya upangaji na ujenzi wa zahanati, vituo vya afya na hospitali. Ushauri wangu ni kuwa suala hili lisimamiwe na Wizara ya Afya ambayo katika busara ya kawaida watatumia weledi kupanga maeneo ya taasisi hizo. Nikirejea ujenzi, uboreshaji wa zahanati na vituo vya afya katika Jimbo langu, inasikitisha kuona kuwa maeneo ambayo yalipashwa kupewa nguvu baada ya wananchi kuonyesha juhudi kwa kujenga maboma hayajafikiriwa. Hii inaonyesha ukosefu wa utaalamu katika kubaini wapi paendelezwe, kwani maeneo mengine yanaachwa bila huduma.

Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Wizara ipitie ujenzi wa zahanati 12 zilizojengwa na wananchi kwa kipindi cha miaka mitatu ili tupate somo juu ya haja ya kuendeleza zahanati na vituo vya afya kwa ulinganifu na kwa kuzingatia zaidi mahitaji, lakini zaidi Serikali itusaidie kwa kuendeleza angalau Zahanati za Rutoro, Bumbire na Crogllo kati ya zahanati hizo 12 kwa kuanzia.

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo lingine la kuangalia ni upangaji wa wataalamu wa sekta ya afya. Ili kuepuka tatizo la sasa ambapo sasa kila wizara inataka watendaji wanaohusika na sekta zao walioko katika Halmashauri za Wilaya wawajibike Wizarani. Wizara ya Afya na TAMISEMI wapitie upya usimamiaji wa watendaji hawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa hii ni Serikali moja, unaweza kuwepo utaratibu ambapo wataalamu wa Wizara ya Afya wanaweza kupata miongozo tokea Wizara ya Afya ikiwa ni pamoja na kupata stahili zao wakiwa Halmashauri za Wilaya. Uwepo wa zahanati wa vituo vya afya ambavyo havina wataalamu ni kutokana na upungufu tu wa msimamizi (DED) kutokuwa na uelewa wa mguso wa sekta.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na umakini wa Serikali katika kutoa vibali vya kuajiri, naomba na kushauri vibali vya kuajiri watendaji wa sekta hii ni muhimu vitolewe. Hii italeta umaana wa kujenga miundombinu ya zahanati, vituo vya afya na hospitali.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho lakini siyo kwa umuhimu, nichukue fursa hii kupongeza msimamo wa Serikali katika kuwasimamia watendaji wa Sekta ya Afya. Siyo busara kwa kila atakayesimama amwelekeze na kumkemea Nurse, Daktari au Mtendaji wa Afya. Kazi nyingine unaweza kuzifanya kwa sababu unajua kongea. Sekta ya Afya watendaji wake wanatumia muda mwingi shuleni, wanahitaji utulivu na wanashughulika na afya na uhai wa binadamu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.