Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, afya ni nguvu kazi ya Taifa lolote. Kamwe Tanzania ya Viwanda haitawezekana kama wananchi wake hawana huduma bora za afya. Pamoja na unyeti na umuhimu wa afya bado Wizara hii imetengewa fedha kidogo sana. Pamoja na Bunge lako Tukufu kupitisha zaidi ya trilioni moja, lakini zilizoenda za maendeleo ni 16% tu. Hii haiendani kabisa na ubora wa afya kwani, miradi mingi imekwama, lakini pamoja na upungufu huo bado fedha zinapungua hadi bilioni 866.2. Hali hii haina ishara njema kwa afya zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na watumishi wachache na kufanya kazi kwenye mazingira magumu bado viongozi wa kisiasa na Kiserikali wasio na taaluma hii wamekuwa wakiwadhalilisha kwa ama kuwasimamisha kazi au kutaka kujieleza mbele ya wananchi. Hivyo, ni muhimu tabia hii mbaya ya kuwa-demorolise madaktari wetu wanaopatikana kwa gharama kubwa sana iachwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, UKIMWI una uhusiano mkubwa sana na TB. Ni kama vile suala la TB halishughulikiwi sana. Hii ni hatari kubwa kwa kuwa, mgonjwa wa TB mmoja asiyetibiwa anaweza kuambukiza watu 10 – 20 kwa mwaka, lakini mbaya zaidi 40% ya wagonjwa wa UKIMWI pia, wana TB. Hivyo magonjwa haya yana mahusiano makubwa basi uzito unaopewa UKIMWI pia, uwekwe kwenye TB.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri nasaha ni muhimu sana hasa ikizingatiwa binadamu lazima akumbane na changamoto za maisha. Hivyo, ni muhimu kitengo hiki kupitia Idara ya Ustawi wa Jamii kujipanga kimkakati kuona ni jinsi gani watakavyotoa huduma hii hata ikibidi kwa gharama kwa kuwa, kuna wanasihi binafsi (wachache) wanaotoa fedha. Pia, vijana (wanafunzi) wawe wanapewa mafunzo kwa vitendo ili wamalizapo waende kusaidia wananchi wenye sonona na misongo ya akili.

Mheshimiwa Naibu Spika, ndoa za utotoni ni tatizo kubwa sana. Sheria hii ibadilishwe ili iendane na wakati.

Mheshimiwa Naibu Spika, afya kwa wote haina mjadala ni muhimu sana, lakini Mtanzania awe na bima.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuondolewa kwa tozo ya VAT katika pads bado ni kizungumkuti. Pamoja na Serikali kuondoa VAT bado fedha ni zilezile 2,000/= per pct na zaidi suala la je, kwa nini mpaka leo bado gharama ni ileile au zaidi?

Mheshimiwa Naibu Spika, Sera ya Wazee toka 2001 hadi leo haina sheria. Ni lini Muswada wa Sheria utaletwa ili wazee hawa wapate ahueni?

Mheshimiwa Naibu Spika, nchi yetu imesaini mkataba (Abuja Declaration) ambapo kila nchi husika zilikubali kutenga asilimia 15 ya bajeti kuu ya Serikali kugharamia sekta binafsi. Ni jambo la ajabu kwamba, sasa inaonekana Serikali haioni umuhimu huo kwa kuwa, hivi majuzi Waziri wa Fedha alikiri haiwezekani kila mkataba tuutekeleze kama tulivyosaini kwa kuwa, sekta nyingine hazitapata kitu, nazo ni muhimu.